· Lengo ni kuboresha lishe, mapato na usawa wa kijinsia
· Wanawake wa wilaya hiyo wajivunia ongezeko la mavuno
· DED awataka maafisa ugani kuongoza hamasa vijijini
Sehemu ya baadhi ya wanawake wa wilayani Bukombe wakisikiliza mkufunzi katika mafunzo ya kilimo cha kisasa na usawa wa kijinsia yaliyofanyika hivi karibuni ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kimataifa ya mwanamke wa kijijini.
Siku ya
Oktoba 15 ya kila mwaka Tanzania huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mwanamke
anayeishi Kijijini kwa kumpatia mbinu mbalimbali za kujikwamua katika maisha na
kuhimiza usawa wa kijinsia katika jamii.
Mwaka huu
maadhimisho hayo yamefanyika kitaifa Kijiji cha Levolos, kata ya Kimnyaki
mkoani Arusha ambapo yaliambatana na maonesho ya siku mbili kuanzia tarehe 14
hadi 15 Octoba 2023 ambapo TWCC kwa kushirikiana na Shirika la Umoja Mataifa
linaloshughulikia masuala ya Usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake (UN
Women) ilifadhili wanawake wajasiriamali wa vijjini watano kushiriki kupitia
Kupitia "Mradi wa pamoja wa kuongeza kasi ya uwezeshaji Wanawake Kiuchumi
Vijijini (Mwanamke Na Uchumi)"
Kwa mujibu wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake
na Watoto Dkt. Dorothy Gwajina maadhimisho yalienda sambamba na Mafunzo na
Mdahalo juu ya masuala ya Jinsia, Ukatili wa kijinsia, masuala ya Haki za Ardhi
na mabadiliko ya Tabia nchi, Malezi na Ustawi wa Afya, Usalama wa Chakula na
Mpango wa Matumizi ya Ardhi.
Maadhimisho
hayo ni kufuatia Tamko la Umoja wa Mataifa na Azimio Namba 62 la Tarehe 18
Disemba, 2007.
Azimio hilo
lilitambua Oktoba 15 ya kila mwaka kuwa ni Siku ya Kimataifa ya Wanawake Wanaoishi
Vijijini na kuzitaka Nchi Wanachama wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha Siku hiyo.
Siku hiyo
imeanza kuadhimishwa Kimataifa kwa mara ya kwanza tarehe 15 Oktoba, 2018.
Lengo la Maadhimisho ni kutambua na kuuenzi mchango wa
wanawake wanaoishi vijijini hususan katika nyanja zauzalishaji wa mazao ya
Kilimo, kuhakikisha Usalama wa Chakula Kaya na kuchangia Ukuaji wa Uchumi wa
Taifa.
Wilayani Bukombe, Maadhimisho yalifanyika katika viwanja
vya Runzewe Kaulimbiu ikiwa ni “Wezesha Wanawake wanaoishi kijijini kwa uhakika
wa chakula, lishe na uendelevu wa familia”
Afisa
Maendeleo Wilaya ya Bukombe, Benadetha Tehingisa alisema kuwa ya siku ya kilele
Octoba 15 ilitanguliwa na matukio kadhaa yaliyoandaliwa na wilaya hiyo kwa
wanawake wanaoishi kijijini ikiwemo semina dhidi ya ukatili wa kijinsia, kilimo
bora na jinsi ya kujikwamua kiuchumi lengo likiwa ni kuleta usawa wa kijinsia
katika jamii.
Kaulimbiu
inasisitiza umuhimu na nafasi kubwa ya Wanawake wanaoishi vijijini katika
kushughulikia ustawi wa familia ikiwemo ushiriki wao katika kilimo ili
kuboresha lishe ya familia katika jitihada za kukabiliana na utapiamula na
udumavu kwa watoto
Njaa na
matumizi mabaya ya ardhi ni kati ya mambo amabyo yanaongeza ugumu wa maisha kwa
wanawake wanaoishi vijijini.
Akieleza
matumizi sahihi ya ardhi na mbinu ambazo amewapa wanawake wanaoishi kijijini
Afisa Kilimo Kata ya Runzewe Mashariki, Hillary Munyuku alisema ni pamoja na
hatua zinazotakiwa kuachwa kati ya mche na mche, tuta na tuta wakati wa
kupanda, matumizi sahihi ya mbolea na dawa, na wakati sahihi wa kuanza kuaandaa
shamba”
Mkulima Agnes John wa Kijiji cha Mwamakunkwa Kata ya
Iyogelo ililieleza gazeti hili faida za mafunzo yanayotolewa na maafisa kilimo
kuwa ni pamoja na ongezeko la mavuno.
“Tunapewa mbinu za kulima na kupanda kisasa
mbegu zilizobora tofauti na zamani ambapo tulinunua tu mahindi sokoni na
kutupia shambani huku shamba moja tukiwa tunachanganya na mahindi, karanga,
kunde na mihogo humohumo” alisema Agnes akifurahia mavuno ambayo ameanza
kuyapata kutokana na jitihada za halmashauri ya Bukombe
Katika
kuhakikisha Kauli Mbiu ya mwaka huu inatekezwa kwa vitendo na wananchi wa
wilaya ya Bukombe wanamudu mahitaji ya kaya ya milo mitatu kwa siku, Mkurugenzi
wa wilaya hiyo Lutengano Mwalwiba aliwataka maafisa kilimo, mifugo na uvuvi wa
wilaya hiyo kuanzia ngazi za vijiji na kata kuongeza ubunifu katika maeneo yao
ya kazi na kuaanda mpango wa kushirikiana na wakulima kuongeza uzalishaji.
Kwa upande
wake Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi,
Zedekia Solomoni aliwataka maafisa ugani kuhakikisha wanawahamasisha pia
kilimo cha pamba ili kila kaya ilime angalau hekari mbili.
“Ardhi, au tuseme kilimo ni nyenzo muhimu kwa Maendeleo ya Mwanamke wa Kijijini. Asilimia 80 ya watu wote wanaishi kijijini na wanawake ni wengi ambao tunaamini ndiyo wazalishaji wakuu wa chakula”. Anaeleza Mkurugenzi wa Sauti ya Wanawake Ukrewe, Sophia Donald
Sophia
alifafanua kuwa mchango wa mwanamke wa kijiji unaweza kusionekane moja kwa moja
kutokana na mila na tamaduni zinazomzunguka.
Alitoa rai
kwa maadhimisho hayo kutumika kuibua mjadala wa wadau mbalimbali kiwemo
Serikali kuweka mazingira mazuri ya umiliki wa ardhi kwa mwanamke wa kijijini
kiwemo marekebisho kwenye sharia ya mirathi.
“Mwanamke akiwa na uhakika wa ardhi kunamuongezea uhakika wa chakula cha kutosha pamoja na uhakika wa kipato na hivyo kupunguza ukali wa matendo ya ukatili kwa kukosa maamuzi dhidi ya kile wanachozalisha” alisema Mkurugenzi huyo wa Sauti ya Wanawake Ukerewe, Sofia
Wakati umaskini kwa ngazi ya ulimwengu ikielezwa kupungua kwa kiasi Fulani, bado watu wengi wanaendelea kuishi katika hali za umaskini wa kukithiri hasa katika maeneno ya vijijini japokuwa ndiko hutegemewa zaidi kwa uzalishaji wa kilimo wa karibia asilimia 80 za chakula barani Kusini mwa Jangwa la Sahara na kuwezesha kusaidia watu wengi wakiwemo wa mijini.
Afisa
Maendeleo ya Jamii, Anna Athanas alieleza hali ilivyo katika jamii kuwa katika
sekta ya kilimo, wanawake wanaweza kuwa na tija na biashara kama wenzao wa
kiume, lakini wana ufikiaji mdogo wa ardhi, mikopo, masoko na kupata bei ya
chini kwa bidhaa zao.
Aidha, inaelezwa kuwa vizuizi vya kimuundo na kanuni za
kijamii bado ni za kibaguzi na zinaendelea kupunguza jukumu la wanawake katika
familia na jamii za vijijini.
“Wanawake na wasichana hawana ufikiaji sawa wa rasilimali
na bidhaa, huduma za umma kama elimu, huduma za afya na miundombinu, na kazi
zao nyingi hazionekani na hazilipwi” yananukuliwa baadhi ya machapisho
mtandaoni.
Kwa ngazi
ya Ulimwenguni, isipokuwa chache, viashiria vyote vya jinsia na maendeleo
ambavyo takwimu zinapatikana zinaonesha kuwa wanawake katika maeneo ya vijijini
wanaishi bila usawa katika hali ya umaskini, kutengwa na wanaathiriwa zaidi na
mabadiliko ya tabianchi kuliko wanaume.
Mabadiliko ya tabianchi huathiri ustawi wa wanawake
na wanaume kwa njia tofauti katika suala la uzalishaji wa kilimo, usalama wa
chakula, afya. Ripoti kadhaa zimeeleza kuwa katika maeneo ya vijijini mara
nyingi wanawake ndio wa kwanza kuhathirika uharibifu wa maliasili na kilimo.
Wanawake vijijini wanapaswa kupewa mbinu mpya za kulima
kisasa ili kuboresha lishe kwa kuhakikisha milo mitatu katika ngazi ya Kaya,
kwa ajili ya lishe bora ya familia na baadaye kuweza kuuza ziada na kuboresha
kipato. Wanawake vijana wanahitaji kupata pembejeo za kilimo ili waweze kulima
kadiri inavyowezekana.
Comments
Post a Comment