Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Tanzania imetoa Kalenda ya mihula ya masomo kwa shule za awali, msingi na sekondari kwa mwaka 2024
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara, muhula wa
masomo unatarajiwa kuanza Januari 8 na kukamilika Desemba 6, 2024.
Aidha, taarifa hiyo imeeleza kuwa kutakuwa na jumla ya idadi
ya siku za masomo 94 katika muhula wa kwanza utakaokamilika May 31 na siku 100
katika muhula wa pili utakaoanza Julai Mosi
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imesisitiza
utekelezaji wa Mihula ya Masomo kwa Mwaka 2024, kwa kuzingatia Kalenda hiyo ili
kuepuka changamoto ya kutokamilisha ufundishaji na ujifunzaji wa mada kwa
wakati.
Wizara imewatakia watu wote maandalizi mema na heri ya Mwaka
mpya wa Masomo.
Comments
Post a Comment