Katika mwendelezo wa kampeni za uchaguzi mkuu, viongozi mbalimbali wanaendelea kumimiinika kwenye mikutano ya hadhara kumu unga mkono mgombea Urais wa chama cha mapindunzi (CCM),Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Bukombe mkoani Geita leo amesisitiza dhamira ya serikali kuboresha sekta ya madini ili iwe na manufaa zaidi kwa wananchi na taifa kwa ujumla ,amesema serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wachimbaji wadogo wakiwemo wafanya biashara wa madini ,ili kuongeza uzalishaji na mapato.Aidha, ameeleza kuwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara za ushirombona katoro ni kipaumbele kwa lengo la kurahisisha usafiri wa watu na bidhaa hivyo kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika wilaya Bukombe.Vilevile amebainisha mpango wakujenga chuo cha ufundi katika eneo hilo ili kuongeza fursa za mafunzo kwa vijana na kuwawezesha kupata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa.
Kwaupande wake Mh Dkt Doto Biteko ameeleza kuwa naimani na mama Samia kutokana na utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo katika jimbo la Bukombe ,maana lilikuwa nyuma kimaendeleo na sasa maendeleo yanaonekana kwa wazi bila shaka yoyote,ikiwemo ujenzi wa miundombinu,upanuzi wa huduma za afya na elimu pamoja na kuimarisha uchumi wa wananchi wa kipato cha chini,uteuzi wake ni kielelezo cha uongozi wa hekima ,uwajibikaji na uthubutu.
Hata hivyo ndugu Anton Mavunde ambae ni Waziri wa madini ameeleza kuwa wachimbaji wadogo wadogo wa madini wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiweo ukosefu wa mitaji ya kutosha,teknolojia duni ya uchimbaji,ugumu wa kupata masoko ya uhakika kwa madini wanayoyapata,kuna haja ya serikali na wadau wa maendelao kuongeza uwekezaji katika mafunzo ya uchimbaji bora,upatikanaji wa mitambo ya kisasa kwa mikopo nafuu.
Comments
Post a Comment