DKT. BITEKO ATAJA DHAMIRA YAKE BUKOMBE BAADA YA UCHAGUZI


Na, Irene Makopudo

Katika mwendelezo wa kampeni zake za ubunge, Dkt. Doto Biteko, ameendelea kuvutia  maelfu ya wananchi katika mikutano mbalimbali  ndani ya jimbo lake, amesisitiza kuwa dhamira yake kuu ni kuendeleza miradi ya maendeleo ,kuboresha  huduma  za jamii na kuendelea kusikiliza sauti za wananchi.

Amezungumza hayo na wananchi katika mkutano wa 23 wa kampeni kata ya Bukombe kijiji cha Ikaranga,  ameeleza mafanikio yaliyofikiwa  katika kipindi cha miaka mitano, ujenzi na ukarabati wa shule na zahanati, upatikanaji wa maji safi na salama, kuboresha  barabara za mjini na vijiji."Tumekuja kuomba kura kwasababu tunayo kazi yakufanya kwaajili ya kijiji na kitongoji, tunayo kazi yakubadilisha hali na maisha  ya watu kwa kuleta maendeleo kwenye maeneno haya, Ikaranga ninayo ijua mimi  ya miaka kadha niliyo ijua mimi, Ikaranga ambayo tulikuwa tunachukua muda kubishana, Ikaranga ile imekwisha badilika,"alisema Dkt. Biteko.

 Dkt. Biteko ameeleza mafanikio ambayo yamepatikana katika kipindi chote ndani ya  miaka mitano, kuwa Ikaranga haikuwa na umeme, barabara, maji, lakini kwasasa  kuna barabara, umeme, shule, na maji, amewasisitiza wananchi  kwenda kupiga kura siku itakapo fika maana maendeleo hayaji bila kupiga kura wananchi wajitokeze kwa wingi siku hiyo ya Oktoba 29,2025.Kwaupande wake mgombea udiwani kata ya Bukombe Rozalia Masokola aliwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwenye mkutano huo na kuwataka kujitokeza Oktoba 29 mwaka huu kupiga kura kwa wingi ili maendeleo ya wepo katika kata hiyo  lazima watu wajitokeze siku ya kupiga kura, maendeleo  yetu ni kura  yako.

 

Comments