DKT. BITEKO AMEENDELEA KUSAKA KURA ZA CCM


Na, Irene Makopudo

Mgombea ubunge  Dkt Doto Biteko  anaendelea na kusaka kura katika wilaya  nzima Bukombe  katika kata na vitongoji vyote vya Bukombe.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Bweda kata ya Namonge waomba wananchi kujitokeza kwa wingi  kupiga kura na watakapopiga kura  hiyo maana yake ni kutimiza wajibu wao wa kidemokrasia ambao utawawezesha kutimiziwa  mahitaji yao ya kijamii.

Dkt. Biteko Katika mkutano wakampeni akiomba kura za Rais Dkt. Samia na udiwani ameeleza utekelezaji wa Ilani ya chama cha mapindunzi katika miaka mitano  iliyopita ambapo utekelezaji wake umekuwa mkubwa ,katika kata  ya Namonge na vitongoji vyake.

"Nataka nianze kwa kuwashukuru kwa ushirikiano ambao mmetupatia katika miaka mitano iliyo pita kama viongozi wa wakilishiwenu tumeona raha kufanya kazi ya uwakilishi  kwanini?, kwasababu hakuna jambo tumepungukiwa katika kata yenu hii ni kata kubwa kati ya kata 17  katika  wilaya ya Bukombe, ni kata yenye watu wengi na hii ni kata moja wapo,"alisema Dkt. Biteko.Aliongeza kuwa wakati wa uchanguzi katika kipindi kilicho pita ukanda huo wa Namonge ulikuwa ni ngome ya upinza ,ambapo walifungiwa njia ya kupita lakini watu wa Namonge walisimama imara  ile ngome ili vunjwa na upinza haukuwepo tena ,watu waliamini  chama cha mapindunzi (CCM) na kushikamana kwa umoja ili kupata maendeleo.

"Nataka niwaambie kazi tumeifanya  tena kwa nguvu zetu zote  ili tubadilishe hali ya maisha tu, eneo ili miaka iliyopita gemu wakiishiwa hela porini  anakuja kutafuta hela kwa wananchi,watu wakawa wanaishi kwa mashaka,watu wakawa wanakanguliwa mbao hadi kwenye  uvungu wa vitanda vya watu  ,hali ya maendeleo haikuwepo,barabara hazikuwepo, tukitaka kwenda Namonge makao makuu hakuna barabara,"alisema Dkt. Biteko.Sambamba na hayo  ameeleza walimu ambao waliotokea kupangwa katika kata hiyo walilia kwa sababu kulikuwa ni shida,  maji ,umeme ,barabara, hospitali ,kwa ujumla maisha yalikuwa ni mangumu ,maendeleo  ambayo yamepatikana kwasasa ni kutoka kwa Mama Dkt. Samia, barabara zote zitatengenezwa ili watu waweze kusafiri kwa urahisi bila usumbufu tena. Kwaupande wake mgombea udiwani  kata ya Namonge Mlalu Bundara ,aliwapongeza wananchi  na kuwashukuru kwa dhati na kuwaomba wajitokeze siku ya Kupiga kura Oktoba 29 za Rais Samia ,Dkt. Biteko kwa wingi  ili maendeleo yaendelee  katika kata yao ya Namonge.

 

Comments