WANANCHI UYOVU WAJITOKEZE KWA WINGI MKUTANO WA KAMPENI ZA DKT. BITEKO

Na ,Irene Makopudo

Wananchi wajitokeza kwa wingi kumsikiliza Mgombea Ubunge Jimbo la Bukombe Mkoa wa Geita Dkt Doto Biteko kwenye mkutano wake wa kampeni katika kata ya Uyovu  kwa kusikiliza sare. Katika mkutano huo wa kampeni Dkt. Biteko ameahidi maendeleo katika kata ya Uyovu kwa kuifanya Uyovu kuwa ni kata yenye maendeleo ,ameahidi ujenzi wa stendi ya Malori  na bodaboda ili kuepusha ajali ambazo huwa zinajitokeza mara kwa mara katika kata hiyo. "Kata  ya Uyovu ilikuwa haina maendeleo kabisa leo kuna sekondari nyingi na shule za msingi zimeongezeka tunataka tuongeze miundombinu  tunataka tujenge hospitali, nataka niwaambie watu wa Uyovu mna neema ya kuzaa watoto, tumejenga shule  maalum ipo hapa Uyovu na Ushirombo, na stendi ambayo tunajenga lazima iwe ya kisasa,"alisema Biteko.

Ameongeza kuwa Uyovu kuna mradi wa maji ambao unaendelea katika kata ya Uyovu, miaka mitano ijayo Uyovu  itakuwa ya kisasa. 

Vilevile amesema kuna fedha zimetengwa ili kuweza kusaidia vijana na wakinamama kwaajili ya kuwakopesha ili waweze kufanyia  biashara ilikuleta maendeleo katika kata hiyo ya Uyovu ,katika kata hiyo itakuwa jicho la Dkt Biteko kuanzia Januari hadi Desemba. Sambamba na hayo mgombe udiwani Matayo Kagoma aliwapongeza wananchi kwa kufika kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni hizo jinsi wameweza kufika kwenye mkutano ,aliahidi  kuleta maendeleo.

Alisema katika kata hiyo japo maendeleo yapo lakini pia bado yanahitajika  ili kukambiliana  idadi ya watoto ambao wanaongezeka kwahiyo agenda ya kumchangua Dkt. Biteko  ni muhimu kwa maendeleo. 


Comments