MWENYEKI WA CHAMA CHA MAPINDUNZI CCM AZINDUA KAMPENI KATA YA IGULWA

 
Na Irene Makopudo

Mwenyekiti wa chama cha Mapindunzi CCM Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita Ndugu Matondo Lutonja amenzindua kapen za udiwanui  kata ya Igulwa huku akieleza ilani ya chama cha mapindunzi na miradi  ambayo iliyotekelezwa na Mwenyekiti wa chama cha mapindunzi Taifa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hasani.Akizungumza na wakazi wa kata ya Igulwa  ameeleza Ilani hiyo na kumkabizi Ilani ya chama cha mapinduzi diwani Richard Mabenga na kumuombea kura kwa wakazi wa kata hiyo,huku akimpongeza kwa kazi ambazo amefanya za maendeleo kwa jamii  katika kata ya Igulwa.Mgombea udiwani kata ya Igulwa Richard Mabenga  amefafanua utelezaji wa  maendeleo  katika ngazi ya kata ya Igulwa huku akimpongeza  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko  na mgombea ubunge Jimbo la Bukombe kwa maendeleo ambayo ameyafanya katika jimbo  lake huku akitaja miradi mikubwa ya kimikakati inayotekelezwa katika kata ya Igulwa.

Sanjali na hayo ameweza kuitambanaisha katika hadhala hiyo, utekelezaji  wa sekta ya miundombinu ya barabara  za kata  ya Igulwa sekta ya  afya, ongezeko la vituo vya afya na uboreshaji wa vituo hivyo ,sekta ya maji napo wamefanikiwa kuwa na mradi wa maji safi na salama katika kata hiyo ,na katika  sekta ya nishati sasa wakazi wa Igulwa mambo ni safi mno.Amesema vilevile  kata ya Igulwa  katika sekta ya elimu haikubaki nyuma imetekeleza mradi wa shule pamoja na vyuo na katika sekta ya biashara haikuwa mbali imeweza kutekeleza mradi mkubwa wa kimkakati   kwa kuanzisha  unjezi wa mradi wa soko kubwa la kisasa, stendi ya mabasi  na uwanja mkubwa wa mpira wa kisasa.

Comments