DKT BITEKO AENDELEA KUMWANGA SERA ZA CCM KATA KWA KATA

 

Na Irene Makopudo

Mgombea ubunge jimbo la Bukombe ,Dkt. Dotto Biteko  amewataka wananchi wa kata ya  Ng'anzo Wilaya ya Bukombe Mkoani wa Geita kujitokeza kwa wingi  Oktoba 29, 2025 kumpigia kura Dkt Samia Suluhu Hassan  kwa kuwa  anania thabiti ya kuleta maendeleo.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni zake kata ya Ng'anzo katika ameeleza mafanikio ambayo yamefanikiwa kufanyika katika kata hiyo, amesema  miaka ya nyuma hapakuwa na barabara ,umeme ,shule ya sekondari na zahanati. Amesema wananchi wakipoga kura za kishindo Zahanati ya Ng'anzo ita pandishwa hadhi kutoka kwenye zahanati kuwa kituo cha afya.Dkt Biteko amewashukuru wakazi wa kata hiyo kwa kujitokeza kwenye mkutano huo lakini amewahakikishia wakazi wa Ng'anzo  kwamba maendeleo lazima yaendelee kufanyika katika kata hiyo na kuwataka wakazi hao kujitokeza  kupiga kura."Ng'anzo haikuwa hivi haikuwa na barabara ,hapakuwa na sekondari watoto wengi walishindwa kuendelea na masomo kwa sababu ya umbali walishindwa kuendelea na shule wengi walibebeshwa mimba, hospitali  ilikuwa shida wakati wamama wanakwenda kujifungua walikuwa wanajifungulia njiani wakiwa wanaenda hospitali nje ya kata", aisema Dkt BitekoAmeongeza kuwa  endapo mtampa diwani, Mungu Rais wa CCM ridha ya kuongoza tena maendeleo ni lazima ,miaka mitano itakuwa ya maendeleo ,mkoa mzima wa Geita  Wilaya inayo ongoza ni Bukombe katika sekta ya elimu imeongoza kuanzia darasa la 4, darasa la 7  na sekondari hadi kidato  cha 6 .Awali mgombea udiwani wa kata ya Ng'anzo Mashaka Shing'wenda ameeleza maendeleo ambayo yamefanyika kata hiyo ,katika sekta  mbali mbali zikiwemo miundombinu ya barabara  kutoka Ng'anzo hadi Bulenga kilomita 6 na Barabara ya Mtakuja hadi Isemabuna kilomita 4, Mbagwa hadi Butinzya, Mtinga hadi Segwe na Bwenda.Shing'wenda alimshukuru Dkt Biteko  kwa maendeleo ambayo wamepata katika kata ya Ng'anzo ,kwasasa maji yapo na umeme upo, aliwaomba wakazi wa Ng'anzo kupiga kura kwa wingi.


 

Comments