UWT BUKOMBE YAJIPANGA KUTOKOMEZA VITENDO VYA UVUNJIFU WA AMANI


Na zena seleman ,Bukombe

Ameyasema hayo katibu wa UWT  Wilaya ya Bukombe Teddy Magani katika ziara yake ya kikazi  katika kata ya Lyambamgongo Wilayani Bukombe  Mkoani Geita.

 " nipende kuwaomba akina mama wenzangu  kuelekea katika uchaguzi  wa serikali  za mitaa na vitongoji na uchaguzi mkuu 2024_2025  tujikite katika kupinga vitendo vya uvunjaji wa amani ili tuweze kupiga kura na kuchagua viongozi kwa Sheria taratibu na haki kwa kila mgombea." alisema Teddy

Hata hivyo Teddy owaomba wajumbe wa mkutano huo kuweza kumuunga mkono Rais  Samia kuelekea katika uchaguzi mkuu kwa kumpa kura za kishindo Mbunge wa jimbo la Bukombe Dkt. Doto Biteko kutokana na mambo mazuri ikiwemo miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa. 

Kwa upande wake diwani viti maalumu tarafa ya Bukombe pili kondela ambae pia ni mlezi wa UWT kata ya Bukombe  amewaomba wajumbe wa mkutano huo kuhakikisha wana muunga mkono Rais Samia kwa kumpa matunda katika  uchaguzi  mkuu ujao 2024_2025.

Awali Katibu wa UWT  Wilaya ya Bukombe  Teddy mageni ametembelea nyumbani kwa mabarozi 7 waliopo katika kata hiyo ya lyambamgongo  huku akihamasisha watu wajitokeze katika kujiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura.

Comments