Mtoto wa miezi minne auawa na kunyofolewa viungo
Na Henry Evarist, Bukombe
Mtoto mchanga wa miezi minne mwili wake umeokotwa katika kata ya Katome wilayani Bukombe ukiwa umeondolewa mkono na mguu katika mwendelezo wa matukio ya ukatili Julai 25, 2024.
Mwili huo umehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ambapo
bado jina na wazazi wake bado hawajajulikana ambapo mganga mkuu wa wilaya hiyo
(DMO) Deograsia Mkapa alisema mtoto huyo aliyeuawa na wasiojulikana, hana
ualbino.
Kufuatia tukio hilo ambalo polisi mkoa wa Geita wamesema
uchunguzi bado unaendelea, Dkt. Deograsia aliwataka wazazi na jamii kuchukua
hatua za kuwalinda watoto
“Matukio haya siyo hapa Bukombe tu. Matukio yamekuwa mengi
kama ambavyo tumekuwa tukiona yanaripotiwa kwenye vyombo vya habaria katika
maeneo mengine ya nchi. Hivyo natoa wito kwa wanawake kuwalinda wanawake na
watoto” alisema Dkt. Deograsia
Tukio lingine ni mwanamke Rehema Paul (26) aliyenusurika
kuuawa kwa kukatwa na mapanga katika maeneo mbalimbali ya mwili wake katika
eneo la Mnada wa Zamani maarufu kama “Masankuloni” majira ya saa mbili za usiku
alipokuwa akirejea nyumbani kutoka kwa wifi yake mtaa wa Kapela jirani na
anapoishi.
Kiganja cha mkono wa kulia wa Rehema kimehifadhiwa pia chumba
cha maiti baada ya kuondolewa wakati akijikinga na shambulio kichwani huku
mkono wa kushoto na maeneo ya kichwani yakiwa yamejeruhiwa vibaya.
Dada yake Rehema aliyejitambulisha kwa jina la Gaudensia
George aliyekutwa wodini hapo akimuuguza ndugu yake pamoja na kupongeza
jitihada za hospitali ya wilaya katika kunusuru maisha ya ndugu
Aidha, Mwenyekiti wa kitongoji cha Igulwa Kata ya Igulwa,
Lucy Samweli alisema kuwa alipigiwa simu majira ya saa mbili za usiku na
kuelezwa kuwa Rehema amekatwa na kitu chenye ncha kali ambapo alifika na kupiga
simu polisi ambao walifika haraka na kumuwaisha hospitali ya wilaya.
“Kufuatia tukio hili la kusikitisha natoa wito wito kwa
wananchi wangu tujilinde sisi kwa sisi” alisema Lucy na kuongeza kuwa mpaka
sasa watu wane tayari wamekamatwa kufutia tukio hilo.
Jirani wa majeruhi, Joyce Selenda ameeleza kusikitishwa na
tukio hilo kwa kuwa jirani yake Rehema wa kwa mama Esther alikuwa ni mtu
aliyeishi vizuri na majirani.
Hata hivyo, Rehema leo amaeweza kuzungumza na mwandishi wa
Bukombe sasa na kusimulia tukio zima lilivyokuwa akitaja sababu na watu anaohisi
kuhusika (majina yao tunayahifadhi kwa sababu za maalumu) huku deni la kiasi
cha shilingi 10,000 na wivu wa mapenzi vikihisiwa.
Tukio la tatu linahusu mtu mmoja anayekadiliwa kuwa na umri
wa miaka 30-35 ambaye jina lake halikuweza kutambulika mara moja mwili wake
umeokotwa jirani na hospitali ya wilaya ya Bukombe ukiwa tayari umeanza
kuharibika.
Maafisa wa polisi wilaya ya Bukombe wakichukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi na kuuhifadhi
Taarifa za kuonekana kwa mwili huo wa mtu ambaye
ametambuliwa kuwa na matatizo ya akili (chizi) zilipatikana wakati wa
maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yaliyofanyika hospitalini hapo yakiongozwa na
katibu tawala wa wilaya kwa niaba ya mkuu wa wilaya ambao walifika eneo hilo na
mwili kuchukuliwa na polisi na kuhifadhiwa hospitali ya wilaya.
Mganga mkuu alidhibitisha kupokea miili hiyo ambayo ambayo
tayari imehifadhiwa mochwari na kusema kuwa mwili wa mtu mzima aliyeokotwa
umetambuliwa kwani ni mtu ambaye alikuwa akipatiwa matibabu ya matatizo ya
akili mara kwa mara hospitalini hapo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Geita, Sofia Jongo alipopigiwa simu kuthibitisha kutokea kwa matukio hayo
simu yake iliita bila majibu.
Wananchi waliozungumza na Bukombe sasa wamelitaka jeshi la
polisi kuwatafuta na kuwachukulia hatua kali watakaobainika kuhusika katika
matukio hayo ya kikatili.
Comments
Post a Comment