Katibu tawala wa wilaya Bukombe, Aly Mketo (mwenye trakisuti na glavuzi) akiongoza wananchi wa wilaya hiyo kufanya usafi katika hospitali ya wilaya ikiwa ni maadhimisho ya Siku ya Mashujaa Julai 25, 2024
Na
Henry Evarist
Katibu
tawala wa wilaya Bukombe, Aly Mketo ameongoza maadhimisho ya siku ya mashujaa
kwa kufanya usafi hospitali ya wilaya pamoja na mazoezi ya viungo.
Akiongoza kamati ya ulinzi na usalama, wakuu wa idara mbalimbali za halmashauri
pamoja na viongozi wengine mapema leo Julai 25, Mketo kwaniaba ya mkuu wa
wilaya hiyo, Mhandisi Paskas Muragili aliwataka wananchi wote kuwaenzi mashujaa
waliopigania uhuru kwa kufanya matukio mbalimbali ikiwemo usafi na utunzaji wa
mazingira pamoja na kuwaombea waliotangulia mbele ya haki.
"Lengo la siku hii ni kuwakumbuka wapambanaji wetu waliomwaga damu nyingi kwa ajili ya kudai uhuru wakiwemo Mwalimu Nyerere na Karume. Katika harakati za kudai uhuru mashujaa wetu baadhi walimwaga damu wakipigania taifa ili ikiwemo vita ya majimaji, hivyo lazima tuwaenzi na kila mmoja kwa Imani yake kuwaombea dua na maombi" alisema Mketo
Katibu tawala wa wilaya Bukombe, Aly Mketo (katikati) akizungumza na watumishi wa wilaya ya Bukombe (Hawapo pichani) baada ya kumaliza kufanya usafi na mazoezi katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa Julai 25, 2024 katika hospitali ya wilaya
Aidha
aliwataka vijana na watu mbalimbali kuwa na moyo wa uzalendo pamoja na kujitoa
kwa ajili ya maendeleo ya nchi yao.
Kwa
upande wake mjumbe wa kamati ya usalama ya wilaya ya Bukombe ambaye pia ni
mkufunzi wa Jeshi la Akiba, Staff Sargent Juma Magembe aliwataka vijana
kujiunga kwa wingi katika jeshi hilo ili kutoa mchango wao kwa taifa
Mganga Mkuu wa halmashauri ya Bukombe, Dkt.
Gaudensia Mkapa aliwashukuru wote walishiriki katika usafi wa hospitali ya
wilaya akisema ni upendo mkubwa kwa wananchi wanaopata huduma hospitalini hapo
kuwa imewaongezea morali wa kufanyakazi.
Wakizungumzia maadhimisho hayo, wananchi waumepongeza uongozi wa wilaya hiyo
kwa kuadhimisha siku hiyo muhimu
"Vijana wanapoona matukio kama haya inawatia moyo na kuona kuwa taifa hili
wapo waliolipigania na hivyo nao kuvutiwa na kuwa tayari kutumika kwa faida ya
wengine" alisema Hussein Masanja mkazi wa kata ya Katente
Baadhi ya Vijana wilayani Bukombe wakishiriki zoezi la usafi wa
mazingira katika hospitali ya wilaya katika kuadhimisha Siku ya Mashujaa Julai
25, 2025
Naye
kijana Juma Mstapha kutoka kata ya Igulwa alieza kuvutiwa na maadhimisho hayo
akiahidi mwakani kushiriki kimamilifu.
“Hii
ni heshima kwa mashujaa wa taifa hili na kila kijana angetamani kuwa historia
ya nchi yake hivyo hata kushiriki matukio kama usafi katika maeneo ya umma na
kusikiliza hotuba mbalimbali za viongozi ni jambo linazidi kunipa hamasa ya
kutumikia taifa langu Tanzania” alimalizia Juma katika mahojiano na mwandishi
wa habari hii.
Comments
Post a Comment