KAMATI YA USHINDI UWT BUKOMBE YAJIPANGA VYEMA USHINDI NI LAZIMA 2024_2025



Na zena Selemani, Bukombe 

Ameyasema hayo katibu wa UWT Wilaya ya  Bukombe Teddy Mageni wakati wa ziara yake ya kuwapa semina ya uongozi makatibu wa UWT ngazi zote katika kata ya uyovu Wilayani Bukombe mkoani Geita.

,,sisi wanawake ni jeshi kubwa naimani tutafanya vyema katika uchaguzi mkuu wa Serikali za vijiji na vitongoji  mwakaa huu naimani hatutamuangusha Rais Samia na mbunge wetu Dkt. Doto Biteko  kwa sababu sisi wanawake tukiamua tunaweza."alisema Teddy

Hata hivyo Mageni waliwasihi wanawake  wajitokeze katika uchaguzi  wa serikali za mitaa,vijiji, na vitongoji na uchaguzi mkuu 2024_2025 kwaajili ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi .


Naye katibu wa UWT kata ya uyovu Mariamu Amri alisema jumuiya ya wanawake UWT  imekuwa chachu ya maendeleo  katika jamii kumekuwa na maendeleo  mengi yaliofanywa  kupitia jumuiya hii hata hivyo pia tunamshukuru sana Dkt Doto Biteko Mbunge wetu, Naibu waziri mkuu na waziri wa nishati, amekuwa kiongozi mwema sana  na ameleta maendeleo makubwa sana ikiwemo kunjenga, zahanati , shule, na vituo vya afya ndani ya wilaya yetu kwa ujumlaaa.
Awali katibu muhtasari Wilaya ya Bukombe Anastazia pius aliwafundisha makatibu hao wa matawi na kata jinsi ya kuanda mihutasari ya vikao kutokana na na makatibu hao wengi wao kuto kufahamu jinsi ya kuaanda mihutasari ya vikao vyao .

Comments