ASKOFU MKUU KANISA LA PENTEKOSTE TANZANIA AWATAKA WAKRISTO KUENDELEA KUMUOMBEA RAIS SAMIA NA WASAIDIZI WAKE

 

Askofu mkuu wa kanisa la Pentekoste Tanzania  Eliaza Issaka amewataka wakrsto kuendelea kumuombea Rais Samia na wasaidizi wake  ili Mungu awalinde waendelee kuwatumikia wa Tanzania kwa kuwaletea maendeleo. 

Ameyasema hayo katika ufunguzi wa kongamano la wanawake wa kanisa la Pentekoste  Tanzania llilofanyika  Runzewe mashariki wilayani  Bukombe  Mkoani  Geita. 

Askifu Issaka aliwaomba waumini kuendelea kutendamema kwa kuiunga mkono Serikali kwa kuielezea mazuri inayofanya.

" Nakuomba M/K wa  UWT Mkoa wa Geita utufikishie salamu kwa Rais Samia  asiwe na wasiwasi kabisa achapekazi na uchaguzi ukifika achukuwe fomu sisi kama ma Askafu tukishapitisha hakuna atakae pinga alisema Issack".


Kwa upande wake mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Geita Lolesia Bukwimba  amewataka wanawake kujitokeza katika uchaguzi  mkuu na uchaguzi wa Serikali  za vitongoji kwa kugombea nafasi mbalimbali  huku akiwataka wamuombee Rais Samia kutokana na kazi nzuri anazozifanya

" niwaombe  wanawake wezangu tujitahidi kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi  mkuu na uchaguzi  wa Serikali  za vijiji na vitongoji  kwa lengo la kumuunga mkono Rais Samia, "alisema Bukwimba.

Katibu wa umoja huo wa wanawake wa pentekoste Tanzania  Estar Emmanuel  akisoma taarifa alisema kongamono hilo tangu limeanza lina miaka 10 na limenufaisha wanawake  wengi ikiwemo kujikita katika maombi na kuwafanya wakina  mama wengi kuwa na malezi  bora katika familia zao. 
Alisema kongamano  hilo litakuwa ndani ya siku sita ikiwa lengo ni kufundisha wanawake  malezi bora na kujikita katika maombi ya kiroho ikiwemo kuiombea Serikali.

Comments