UWT YAPIGA MARUFUKU WAGOMBEA KUJINADI NA KUTOA VITU KWA WAPIGA KURA KABLA YA MUDA WA KAMPENI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU SERIKALI ZA VIJIJI NA VITONGOJI 2024

 


Na Zena seleman

Ameyasema hayo katibu wa uwt wilaya ya  Bukombe Teddy Mageni wakati wa ziara ya kikazi ya kamati ya utekelezaji  wilaya  ya kuhamasisha na kukagua uhai wa chama na jumuiya ya uwt katika kata ya igulwa wilaya Bukombe Mkoani Geita.

" Nimarufuku  wagombea mnaotarajia kuchukua fomu za kugombea  uongozi wa wenyeviti wa serikali za vijiji na vitongoji kufanya kampeni na kugawa vitu vikiwemo kanga, chumi, na vitu kwaajili ya kutafuta kura ukibainika hatutakuacha salama"alisema Teddy

 Akisoma taarifa ya kata ya Igulwa kefleni Edson alisema hali ya kisiasa ipo shwari na tayari wanawake wengi wamejitokeza na kuchukua kadi  za jumuiya ya uwt na kusajiliwa Katika mfumo wa kieletroniki 



Na hivyo wanataraji Mambo mazuri na hawatamuangusha mhe Rais  wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan  katika uchaguzi wa serikali za vijiji  na vitongoji .


Diwani wa kata ya Igulwa Simon Mabenga kwa niaba ya wajumbe aliwashukuru kamati ya jumuiya ya uwt wilaya ya  utekelezaji kwa kuendelea kuhamasisha na kukagua uhai wa chama na jumuiya ya uwt .


MWISHO

Comments