Dodoma
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Mhe. Dkt Doto Biteko
amewataka viongozi wa dini kutochoka kuunganisha watu ili kujenga Taifa lenye
Umoja, Amani na Mshikamano
Mhe. Dkt Biteko ameyasema hayo kwenye Mkutano wa Baraza la
Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste ambao ulikuwa na lengo la kuombea Amani na
Umoja miongoni mwa makanisa hayo.
Amesema Serikali inathamini mchango mkubwa unatolewa na
Viongozi wa Dini nchini na kutoa wito kwa maaskofu wa Makanisa ya kipentekoste
kuunga mkono jitihada za serikali Kuhakikisha amani inadumishwa.
"Nawapongeza Sana Baraza la Umoja wa Makanisa ya
Kipentekoste kwa Kuwa na Umoja na waumini wengi nchini wanaofikia takrbani
milioni 12, pamoja na Umoja wenye nguvu na mshikamano" Alisema Dkt.
Biteko.
Awali akizungumza kabla ya mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Umoja
wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania-CPCT Askofu Dkt Barnabas Mtokambali,
amesema Kuwa, viongozi wa dini wanathamini jitihada zinazofanywa na Mhe. Rais
Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Kuhakikisha
demokrasa, utawala Bora na Amani inadumishwa hapa nchini
"Tunaipongeza Serikali kwa kazi nzuri inayofanya
kuhakikisha nchi iko kwenye utulivu, ustawi na amani na kuahidi kutoa
ushirikiano pamoja na kuiombea Serikali
Mkutano wa Baraza la Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste
Tanzania ulianzishwa miaka thelathini iliyopita na ina jumla ya waumini milioni
12, na tayari madhehebu 28 yako mbioni kujiunga na Umoja huo wenye jumla ya Wanachama 128.
Mkutano huo wa Umoja wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste
CPCT umehudhuriwa na Mwenyekiti wa kwanza wa Umoja huo Askofu Dkt. Sylvester
Gamanywa, Makamu Mwenyekiti wa CPCT Askofu Dkt. Daniel Awet, pamoja na Maaskofu kutoka Madhehebu
mbalimbali Chini ya Umoja huo.
Comments
Post a Comment