WAZIRI wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angelina Mabula amewaagiza Wakurugenzi
wote wa Mamlaka za Serikali za mitaa kupima, kulinda na kusimamia
maeneo yote ya umma na maeneo ya wazi ili kuondokana na
mwenendo mbaya unaoendelea kukithiri wa kuvamia maeneo hayo.
Agizo hilo alilitoa leo jijini hapa kwenye mkutano mkuu wa Nane wa mwaka wa bodi ya usajili wa wataalamu wa Mipango miji ambapo alisema kumejitokeza utaratibu mbaya na usiovumilika, wa kuvamia maeneo ya wazi, maeneo ya umma pamoja na maeneo hatarishi na kuyabadilisha kuwa ya matumizi mengine, hasa makazi.
Amesema Maeneo hatari kimazingira pamoja na maeneo ya wazi, yakiwemo maeneo maalum kwa matumizi ya baadaye (land bank), yanapaswa kupimwa, kumilikishwana kulindwa dhidi ya wavamizi.
Alisema ili tuwe na miji nadhifu na iliyopangwa vyema katika nchi yetu hakuna budi kuanza kusimamia upangaji wa miji midogo na vitovu
vya vijiji.
"Takwimu za Sensa ya Watu na Makazi 2022 inaonyesha kuwa miji
inakuwa kwa asilimia 4.8 na taarifa tulizonazo tuna jumla ya miji midogo
inayochipukia 4310 nchini ambayo isiposimamiwa ipasavyo itakuwa miji
holela ya baadae," Alisema
Na kuongeza"Kwa kutambua umuhimu wa miji hiyo na uwepo wa kasi
ndogo ya upangaji wa vijiji nchini, Wizara imeandaa mwongozo wa upangaji
na ujenzi wa nyumba bora vijijini ili kuwezesha jamii yetu kuanza kupanga
maeneo yao kuanzia vijijini," alisema waziri Mabula
Aidha alitoa maelekezo kwa Bodi ya Usajili wataalam wa Mipangomiji na wanataaluma wote kuweka mkazo Zaidi katika namna ya kuzuia miji yetu midogo na vijiji kuwa makazi holela yabaadae
kwa kusimamia na kuelimisha jamii matumizi ya mwongozo wa upangaji na
ujenzi wa nyumba bora vijijini.
Pia alisema Serikali itaendelea na jukumu lake la kuimarisha
mahusiano ya kitaasisi ili kuimarisha maendeleo ya miji pamoja na kupata
fedha kwa ajili ya kupanga na kusimamia miji.
Hata hivyo alielekeza kuwa gharama za kuweza kumudu kupanga,
kupima na kumilikisha maeneo yote nchini ni kubwa,Ninaelekeza Mamlaka
za Upangaji nchini kutenga fedha kutokana na mapato ya ndani ya kila
mwaka, kwa ajili ya kazi ya kupanga,kupima, kumilikisha,kuendeleza
na kusimamia miji katikamaeneo yao.
Akiongelea suala la Mabadiliko ya tabia ya nchi waziri Mabula alisema Ni suala muhimu sana kwa sasa katika sayansi ya usanifu wa miji duniani kote.
" Ili kukabiliana na
mabadiliko ya tabia nchi katika miji yetu tunatarajia mchango mkubwa sana
wa Wataalam wa Mipangomiji katika kuweka mifumo wezeshi kwa ajili ya
kukabiliana na majanga mbalimbali kuanzia katika usanifu wa mipango
kabambe ya Miji na mipangokina ya usimamizi wa uendelezaji wa Miji," alisema Waziri Mabula
Aliekeza katika suala la kuhimili janga la mafuriko mijini inahitajika, siyo tu
kuimarisha uwekaji wa miundombinu kama mifereji ya maji yamvua, bali pia
kuwekamiundombinu ya kijani kama vile maeneo chepechepe, maeneo ya
Bafa (Buffer zones), mabwawa ya kuzuiamaji ya mvua (detention ponds)
pamoja na maeneo ya kuwezesha maji kuzama ardhini (porous pavements)
ili kupunguza kasi na madhara ya mafuriko.
"Napenda nisisitize kuwa Maafisa Mipangomiji mmepewajukumu kubwa sana la kuongoza mwonekano wa miji yetu na vijiji kupitia taaluma mniyonayo. Ni matumaini yangu jukumu hilo mtalibeba kikamilifu na kuwa wabunifu katika utekelezaji wa majukumu yenu ya kila siku na kuzingatia kikamilifu matumizi ya takwimu mbalimbali za Sensa ya Watu na Makazi, Sensa ya majengo na takwimu nyingine kwa ajili ya kuwezesha utendaji kazi wenu kikamilifu," alisema
Na kuongeza kuwa "Naelekeza bodi ya Usajili Wataalam wa Mipangomiji kuongeza kasi na kuboresha mifumo
itakayowezesha upimaji wa utendaji kazi wa kampuni na wataalam katika
kutekeleza majukumu yao ya kila siku," alisema waziri Mabula
Watumishi na kampuni zitakazofanya
vizuri katika upangaji mwone namna ya kuwapatia motisha na kujenga
ushindani mzuri katika upangaji na usimamizi wa miji ili kuwa na miji salama, Jumuishi, stahimilivu na endelevu.
Pia Alisema Kwamba moja ya mahitaji makubwa katika upangaji wa miji endelevuna himilivu ni pamoja na upatikanajiwa takwimu sahihi zinazoendena na wakati. Ni wazi kwamba umuhimu wa
takwimu hizi unajitokeza wakati wa kutoa maamuzi katika kipindi cha
upangaji wa miji.
Ni muhimu kujua idadi ya watu katika eneo la upangaji ili
kujua ni mahitaji gani ya kijamii yanahitajika katika eneo hilo, kwa mfano
idadi ya shule za msingi, shule za awali, zahanati, vituo vya Afya, maeneo
ya kuchezea watoto Kwa kuwa sensa ya watu na makazi imefanyika
August, 2022 ni vyema sasa takwimu hizo zitumike katika upangaji mipango
ya uendelezaji miji.
Aidha, takwimu za umri, jinsi, idadi ya nyumba, idadi ya
wakazikatika nyumba nk, zinatumiwa na wataalam wetu wa Mipangomiji
katika kupanga mahitaji muhimu ya kijamii miongoni mwa rika mbalimbali,
ikiwemo makazi ya wazee, mahitaji ya shule za awali, shule zaMsingi,
Sekondari, mahitaji ya wenye ulemavu Takwimu na taarifa hizo zote
zinapatikana kutoka katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi.
"Miji ni eneo mojawapo katika kuleta maendeleo ya nchi
kupitia uwekezaji wa aina mbalimbali, ingawaje inaendelea kukumbwa na
changamoto mbalimbali ambazo zinasababisha miji yetu kutokutoa
mchango uliotegemewa katika kuimarisha uchumi, kuongeza uhimilivu, na kuwa endelevu," alisema
Na kuongeza "Mijiyetu inaukuaji wa mtawanyiko ambao unaongeza gharama za kuweka miundombinu kama ya maji,umeme, barabara nk, pamoja na gharama zakufuata mahitaji muhimu. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi 2022 tuna jumla ya majengo 14,348.372kati ya hayo asilimia 0.5pekee ndio majengo ya ghorofa," alisema.
Alitoa rai kwa Wakurugenzi wa Mamlaka za Miji, Manispaa na Majijikupanga miji na kuifanya kuwa ya kiushindani kibiashara,kitalii, na kimazingiraili iweze
kuhimili mabadiliko ya tabia nchi, na kuwamiji salama na mahali pazuri
kwa kuishi na kufanya kazi.
Aidha, aliekeza wataalam wa mipangomiji
nchini kusimamia kikamilifu utekelezwaji wa mipango kabambe
iliyoandaliwa katika maeneo yenu na mipangokina ili kuwa na
uendelezaji wa mji unaozingatia mipangomiji.
" Ninyi wataalam wa
mipangomiji mnapaswa kuwa na wivu na taaluma yenu na msiruhusu
kuharibika kwa miji machoni mwenu," alisema waziri Mabula
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga amesema Wizara imejipanga kujikita mwenye Matumizi ya Tehama ambapo Wananchi Sasa wataanza kulipa Kodi ya pango la Ardhi kwa kupitia simu zao za mkonini Kama wanavyolipa Ankara za maji au Ankara zingine.
Amesema kumekuwa na Changamoto kubwa kwa Wananchi kulipa kodi ya pango la ardhi hivyo maelekezo ya waziri wetu Angelina Mabula wananchi wapelekewe huduma kwa kupitia simu zao za mkonini ili kuweza kulipa Kodi hiyo kwa wepesi na urahisi zaidi.
Pia Katibu Mkuu huyo amesema kupitia Matumizi hayo ya Tehama yatasaidia na kuboresha makusanyo na mapato ndani ya wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
"Hapa naomba nitoe msisitizo juu ya Matumizi ya Teknolojia Jambo litakalo saidia kuendana na Kasi ya kukuwa kwa miji na kuendana na idadi ya Watu , " amesema Mhandisi Sanga
Aidha amesema kupitia mpango huo wa Matumizi ya Tehama itakwenda kusaidia kupinguza migogoro ya ardhi kwa Wananchi.
Mwenyekiti wa bodi ya usajili wa Wataalam wa Mipango miji John Lupala Amesemaa jukumu lamsingi la Bodi nikusajili wataalamu wa Mipango miji ambapo katika Kipindi chote Machi 2023 bodi imeweza kusajili 508 ambapo wataalam 36 wamefutiwa usajili kwasababu mbalimbali ukiukwaji wamaadili wa kitaalauma na kubakiwa na wataalamu 472.
Amesema bodi iliweza kusajili makampuni za Mipango miji 100 ambapo kampuni 13 Kutokana na sababu Mbali ziliweza kufutiwa usajili na kubakiwa na kampuni 87 zilizopo hadi sasa
Naye rais wa Chama Cha Wataalam wa Mipango miji Tanzania (TITP) Dkt Juma Matindana niukweli usiopingika muundo uliopo sasa kunamkanganyiko licha ya jitahidi za kuweka mambo sawa kwani wataalamu wapo Wizara na hata TAMISEMI kuwekwa sawa usiwe na ukakasi.
Aidha amesema wataalamu wa Mipango miji wa meshiriki kwa kiasi kikubwa Sana Serikali na binafsi wametumika katika kazi za urasimishaji ambapo mapaka Sasa kunamichoro ya Mipango miji vipande vilivyotambuliwa na kupangwa ni takriban Milioni 2400000.
Tukichukua ule wastani wa kiwanja 150000 hii ni ile project ambayo ni bilioni 360 Lakini ripoti inaonyesha kubeti sio zaidi ya Bilioni 100 Yani 90 mpaka 100 ndio zimekusanywa kwa makampuni yalishirika katika upimaji na upangaji .
Aidha alisema Miradi hiyo imetoa Miradi mikubwa kwa vijana wanaomaliza katika vyuo vya ardhi ambapo Ilani ya Chama inasema hadi ifikapo 2025 wawe wametengeneza ajira zisizopungua Milioni 8
Comments
Post a Comment