HALMASHAURI YA WILAYA YA BUKOMBE YATOA MKOPO WA SH 222.2 MILIONI KWA WANAWAKE VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU

Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe imetoa mkopo wa shilingi milioni 222 kwa vikundi 35 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Ameyasema hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Lutengano Mwalwiba wakati akimkaribisha mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba kukabidhi mikopo hiyo  ya bila riba zikiwemo pikipiki 20 mbuzi  ijko la gesi pamoja na cherehani nne za mfano

Mwalwiba   amesema  Jambo hili lililo fanyika hapa limeelezwa katika ibara ya 32 na section (s) ya chama Cha Mapinduzi  kuelezea kuwa kutakuwa na shughuri za uwezeshaji  uchumi kwa jamii kupitia sehemu mablimbali .

Mwalwiba ameongeza kwa kusema  wao Kama halimashauri wamepewa maelekeza na Sheria ya fedha ya mwaka 2018 sura namba  290 section ya 37( A)inawataka  watoe asilimia 10 katika vikundi mbalimbali  ili vikundi viweze kujiendeleza kiuchumi nakufikia malengo ya kwamba kila mtanzania anafurahia  matunda ya Uhuru ya Nchi yetu.

Naye mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba  amevipongeza vikundi kwa kuweza kupata vigezo na uhalali wa kuweza  kupata mikopo  kwa asilimia Mia nakuweza kuendesha miladi yao  kwa kupitia mikopo hiyo na amesema katika mikopo hiyo haina riba.

Hata hivyo nkumba amevitaka vikundi vilivyopata mkopo  wakati vikiendesha miladi Yao basi viweze kurudisha marejesho kwa wakati maalumu.

Afisa maendelea halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Lita  Kamenya amesema fedha hizo zimetokana na mapato ya ndani ,fedha ya bakaa na fedha za marejesho ya vikundi na leo Kuna vikundi 35 kati ya vikundihivyo  vikundi vya wanawake 20, vikundi vya vijana 21, na vikundi vya watu wenye ulemavu  vikundi 4 .

Mwanakikundi Mahigwe Kajoro ameishukuru Serikali kwa kuweza kuwawezesha mkopo hivyo kutaweza kuwainua kiuchumi kutokana na mwanzoni alikuwa anaendesha daladala ya baisikeli na kipato chake kilikuwa shilingi 5000 kwa siku Ila kwa Sasa anamakadirio ya  ya kuapata shilingi elfu 30 kwa siku 

MWISHO

Comments