Orodha ya milima mirefu duniani

Mlima Everest ukitazamiwa kutoka upande wa kaskazini

Mbinu inayotumika mara nyingi ni kutaja tofauti kati ya usawa wa bahari na kimo cha kilele cha mlima. Lakini inawezekana pia kutumia mbinu tofauti zitakazoleta matokeo tofauti.

Mlima mrefu kutoka usawa wa bahariEdit

Mlima mrefu duniani kwa kuangalia kimo juu ya uwiano wa bahari ni Mlima Everest ulioko kwenye mpaka baina ya Nepal na China. Kilele chake kipo mita 8,848 juu ya usawa wa bahari. Mlima Everest ni sehemu ya milima ya Himalaya. Pamoja na Everest kuna milima mingine 13 inayopita kimo cha mita 8,000, yote iko katika Himalaya na milima jirani ya Karakoram ambayo ni tokeo la kukunjwa kwa ganda la dunia tangu bamba la Uhindi lilianza kugonga bamba la Ulaya-Asia.

NafasiKileleMita juu ya usawa wa bahariMilimaNchi
1.Mlima Everest
(Kitibet Chomolungma, Kinepali Sagarmatha)
8,848HimalayaNepalChina (Tibet)
2.K2 (Kichina Chogir)8,611KarakoramPakistan, China (Xinjiang)
3.Kangchenjunga8,586HimalayaUhindi (Sikkim), Nepal
4.Lhotse8,516HimalayaNepal, China (Tibet)
5.Makalu8,485HimalayaNepal, China (Tibet

Comments