Waheshimiwa Madiwani wakifuatilia taarifa za miradi ya maendeleo kwenye makabrasha
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bukombe Mkoani Geita Yusuph Mohamed amewaomba Madiwani kuendelea kuhamasisha wananchi kuendelea kuchagia nguvu zao katika miradi ya maendeleo bila kusahau uibuaji wa miradi mipya.
Mohamed ametoa wito huo leo Machi 30, 2021 kwenye kikao cha madiwani ambapo Diwani wa kata ya Bulenga Erick Kagoma amesema wananchi uchagiaji unaeda taratibu sana.
Kagoma amesema utekelezaji wa miradi ya maendeleo ujenzi wa bweni la wasichana katika shule hiyo liko katika hatua ya mwisho wanapaua ameiomba Serikali kuleta fedha za vitanda na magodolo ya bweni hilo.
Amesema Shule ya Sekondari
Bulenga inauhitaji wa vyumba vya madarasa 22 huku yaliyopo ni 9 na upungufu ni 13
pia alieleza wananchi wamesha jenga madarasa manne yako usawa wa renta na mengune yakiwa usawa wa madirisha,
Kagoma
amesema wananchi wa Kata ya Bulenga kwa nguvu zao wametengeneza viti na
Meza138 tayari meza 22 zimekamilika na wanatarajia kutumia kiasi cha Tsh. milioni 2.9 ikiwa ni nguvu za
wananchi.
Pia Kagoma ametoa shukrani kwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe ambae pia ni Waziri wa Madini Doto Biteko kwa kuwashika mkono
wananchi kwa kuchangia mabati 220 ya ujenzi wa madarasa katika shule ya Sekondari
Bulenga yaliyogharimu zaidi ya milioni 6.
Comments
Post a Comment