BITEKO AIPIGA JEKI KATA ILIYOBAKI BILA SEKONDARI

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita  Mhe Doto Mashaka Biteko  ameamua kuipiga jeki kata ambayo imebaki nyuma bila kuwa na shule ya sekondari  kati ya kata 17 ambayo nikata ya Nganzo kutokana na wananchi wa ke kubweteka wakisubiri wadau na serikali.

Biteko alifikia hatua hiyo baada ya kufika kwenye Kata hiyo ambapo alikuta ujenzi unachelea na kuendelea kuwafanya wanafunzi  kwenda Kata jirani ya Bulenga  na wengine  kwenda Sekondari ya Butinzya



Biteko akiwa kwenye majengo ya madarasa na kuona hali halisi ya changamoto hiyo ya ukamirishaji  wa vyumba vinne na vya madarasa Ofisi moja na kuchangia  zaidi ya Milioni 9 kwa ajili ya mabati 240 ya kuezekea na gharama za ufundi na misumari

“Wana Bukombe wenzangu tuongeze nguvu katika utekelezaji wa miradi ili tuwe na Bukombe itakayokutwa na vizazi vyetu vijavyo ikiwa katika hali nzuri kimaendeleo”alisema Mhe Biteko

Miongoni mwa Wadau wa Maendeleo wa Wilaya Bukombe Gungu Nsangari aliungana na Mbunge kwa kuchangia mbao zenye thamani y ash 4.5 milioni ambapo Katibu wa CCM Wilaya Bukombe Josephat Chacha alipongeza jitihada za Mbunge Biteko  kwa kuendelea kuwahamasisha wananchi kuchangia maendeleo.

 


Comments