WAZIRI BITEKO AANZA KAZI MADINI

Asisitiza


 Utekelezaji wa Yaliyoanishwa kwenye Ilani ya CCM

 Ataka Ubunifu kuwezesha Uwekezaji Mkubwa

 Ataka Kuhuishwa Sera ya Madini ya Mwaka 2009

 Azuia Urasimu usio na Sababu



Watumishi wa Wizara ya Madini na Taasisi zake wamekumbushwa kuzingatia

maeneo muhimu ya kipaumbele yanayopaswa kutekelezwa kwenye Sekta ya

Madini kama yalivyoanishwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi

(CCM) ya Mwaka 2020-2025, Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania Dkt. John Magufuli aliyoisoma wakati akifungua Bunge la 12 la Jamhuri

ya Muungano Novemba, 2020 na Hotuba aliyoitoa Bungeni Mwaka 2015.


Hayo yamebainishwa Desemba10, 2020 na Waziri wa Madini Doto Biteko katika

kikao chake na Menejimenti ya Wizara na taasisi zake, baada ya kuteuliwa na

kuapishwa tena kuiongoza Wizara ya Madini.



Biteko amewataka viongozi hao kurejea tena maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi ya

CCM ya Mwaka 2015 -2020 ili kuona ni namna gani masuala hayo

yametekelezwa huku kila taasisi ikitakiwa kuhakikisha inayafanyia kazi

maelekezo yote kwa lengo la kuhakikisha Sekta ya Madini inazidi kukua na

kuongeza tija kwa taifa ikizingatiwa kuwa, hivi sasa sekta hiyo imeonekana kuwa

kichocheo cha ukuaji kwa sekta nyingine kiuchumi.


Aidha, Waziri Biteko amesisitiza suala la ubinifu ili kuwezesha kuibuliwa kwa

miradi mikubwa ambayo itapelekea kuvutia uwekezaji mkubwa kutoka nje ya

Tanzania na hivyo kuongeza mchango wa sekta ya madini kwenye maendeleo na

uchumi wa nchi.

Kadhalika, Waziri Biteko amezuia urasimu katika kushughulikia masuala

yanayohusu sekta ya madini akilenga kuweka mazingira bora yatakayowezesha

biashara ya madini kufanyika kwa ufanisi ili kuwezesha matokeo chanya katika

ukusanyaji wa mapato ya serikali ikiwemo kuwezesha uwekezaji katika sekta ya

madini kufanyika bila kuwepo vikwazo visivyokuwa na sababu.


‘’ Kama kuna watu wanataka kuchimba wapewe lesni na wapewe fursa na kama

kuna maoni yanayohusisha taasisi nyingine basi yafanyiwe kazi haraka. Tuwalee

wawekezaji tulio nao ili waendelee kufanyakazi,’’ amesisitiza Biteko.

Ametaka kuwepo kwa mazingira wezeshi yatakayopelekea wafanyabishara na

wachimbaji kufanya shughuli zaokwa amani ili kuwezesha kuzalishwa kwa ajira,

teknolojia mpya za uchimbaji na uchenjuaji wa madini vilevile, kuiwezesha sekta

kuzalisha mabilionea wengi.

Vilevile, Waziri Biteko ametaka kufanyiwa kazi suala la utoroshaji wa madini ili

kuzuia mianya inayopelekea kutoroshwa kwa madini ambalo ameeleza awali

lilianza kufanyiwa kazi vizuri lakini kwa sasa tabia hiyo imeanza kurejea.



‘’ Mwanzo tulikwenda vizuri lakini sasa tabia hii imeanza kujirudia. Kwenye

upande madini feki tumepambana nao na tumekamata mitandao ya watu wa

madini feki,’’ amesema Biteko.


Katika hatua nyingine, Waziri Biteko ametaka kuhuishwa kwa Sera ya Madini ya

Mwaka 2009 ili iendane na matakwa ya sasa akirejea Marekebisho yaliyofanyika

katika Sheria ya Madini ya Mwaka 2010.


‘’ Sera ya Madini ya Mwaka 2009 ni ya muda mrefu. Sera hii ianze kuhuishwa

haraka ili iandane na matakwa ya sasa kama tulivyofanya kwenye Sheria ya

madini ambayo ilitoa nafasi ya kurudisha umiliki wa madini kwa wananchi,’’

amesema Waziri Biteko.


Pia, ametaka suala la kuanzishwa kwa Chama Cha Wajiolojia kupewa msukumo

ili likamilishwe haraka ili kuongeza uwajibikaji wa Wataalam hao katika sekta ya

madini.


Aidha, katika kikao hicho, Waziri Biteko ametumia fursa hiyo kuwashukuru

watumishi wote wa wizara ya madini na taasisi zake kwa kufanya kazi kwa

pamoja kama familia moja na hivyo kuwezesha kupatikana kwa mafanikio

makubwa katika sekta ya madini.


‘’ Kuna wakati niliwaeleza kiu yangu ni kujengwa kwa taasisi imara. Nashukuru

hata wakati sipo kila taasisi iliendelea kufanya kazi zake vizuri. Kiu yangu ni

kuona wizara na taasisi zinafanya kazi kwa pamoja ili tuwatumikie watanzania

na tumalize matatizo ya wadau wetu.,’’ amesema Biteko.


Awali, Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila amempongeza

Waziri Biteko kwa kuaminiwa na kuchaguliwa tena kuiongoza wizara ya madini

na hivyo kutumia fursa hiyo kumkaribisha tena wizara ya madini na kueleza ‘’

mafanikio yote yaliyopatikana ni yetu sote kwani sisi sote tulioongea lugha

moja,’’.

Comments