Biteko Ang’aka Mgodi Kutokufuata Sheria ya Local Content



Imeelezwa kwamba mgodi wa North Mara umekiuka Sheria ya Ushirikishwaji wa Watanzania (locol content) baada ya kutangaza zabuni nje ya nchi na kupata mzabuni kinyume  cha sheria za Madini.


Hayo yamesemwa tarehe 18 Desemba, 2020 na Waziri wa Madini Doto Biteko baada ya kufanya ziara maalum mgodini hapo.


Kanuni za Madini (Ushirikishaji wa Watanzania), 2018 Tangazo la Serikali Na. 2/2018 zinataka wamiliki wa migodi kutangaza zabuni hapahapa nchini na endapo hakuna mtanzania mwenyewe sifa au vinginevyo, zabuni hiyo inatangazwa nje ya nchi na atakaepatikana atalazimika kushirikiana na Mtanzania. Biteko amesema, kwa mujibu wa sheria hiyo, mgodi utakaokiuka utatozwa adhabu ya dola za kimarekani milioni tano. Ameongeza kuwa sheria hiyo inalenga kutoa fursa ya watanzania katika kushiri masuala ya uchumi wa madini.


Country Manager, wa Mgodi wa North Mara, Hilaire Diarra, alikiri kosa kutofuata sheria kwa kuwa walikuwa katika presha ya kutekeleza mradi huo. Diarra ameomba radhi na kwamba wapo teyari kufuata maelekezo yatakayo tolewa na Serikali.


Kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeo ya jamii (CSR), Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila alihoji kuhusu utekelezaji wa (CSR). Meneja Mgodi anaeshughulikia Mahusino Gilbert alisema wametekeleza kwa kujenga madarasa, kujenga visima vya maji na masuala ya afya japo Prof. Msanjila alimwambia hawajafuata utaratibu unao takiwa katika kutekeleza miradi ya CSR.


Kutokana na majibu hayo, Biteko ameuagiza mgodi kuanda mpango wa utekelezaji wa miradi ya CSR na kuwasilisha kwenye mamlaka ya serikali za mitaa ili waipitie na kuidhinishwa teyari kwa ajili ya kutekeleza. Akizungumzia kuhusu masuala ya fidia, Biteko amesema wanaolipwa ni wale wenye haki akisisitiza kuwa utaratibu wa mtindo wa watu ku tegesha hawawezi kulipwa fidia.


Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima, amesema suala la fidia nyamongo linacheleweshwa na wananchi kutokwa na mchezo wa suala ya tegesha. Amesema watu watakao bainika sheria itachukuwa mkondo wake.

Comments