Rais Magufuli Afanya Uteuzi wa Mawaziri Wawili

 



Rais, Dkt. John Magufuli ameteua mawaziri wawili wa Baraza jipya la mawaziri leo, Novemba 13.

Uteuzi huo ni wa Dkt. Philip Mpango kuwa Waziri wa Fedha na Mipango, nafasi aliyokuwa nayo katika baraza lililopita.

Pia, Prof. Palamagamba Kabudi ameteuliwa kuendelea kushika nafasi aliyokuwa nayo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Comments