Waziri
wa Madini Mhe. Doto Biteko amewataka wachimbaji wadogo wadogo na wakubwa kuendelea
kuwa waminifu kulipa tozo za serikali na kuacha tabia za kutorosha madini
hali ambayo imeifanya Wizara hiyo kuvuka lengo la ukusanyaji kodi.
" Mei 31 mwaka huu Wizara imekusanya tsh bilioni 479.9 huku serikali iliipangia Wizara kukusanya Tsh bilioni 470.3 ifikapo Juni 30 mwaka huu nna imani Wizara itakusanya tsh bilioni 500 " Alisema Biteko.
" Mei 31 mwaka huu Wizara imekusanya tsh bilioni 479.9 huku serikali iliipangia Wizara kukusanya Tsh bilioni 470.3 ifikapo Juni 30 mwaka huu nna imani Wizara itakusanya tsh bilioni 500 " Alisema Biteko.
Biteko aliyasema hayo wakati akizungumuza na
wachimbaji wachimbaji wadogo na wakubwa wa madini ya dhahabu kwenye soko la
dhahabu mjini Geita wakati wa ziara yake ya kwenda kukaguwa ujenzi jengo jipya la soko lililojengwa kutokana na fedha za Uwajibikaji wa migodi kwa jamii (CSR) zinazo
changiwa na mgodi wa GGM.
Aidha Biteko
alikemea tozo zisizo za lazima kwa wachimbaji wadogo wadogo zinazo tozwa na
baadhi ya wamiliki wa Leseni na serikali za vijiji huku serikali ilishaondoa
tozo zingine zisizo za lazima ili kuepusha utoroshwaji wa madini.
Pia Biteko
alisema Wizara imesimamia vizuri wachimbaji wadogo licha ya kuwepo changamoto
za ukusanyaji wa kodi mwaka huu kutokana na kushuka kwa uzarishaji kutokana na Mvua nyingi pamoja na janga la Corona.
Kwa upande Mkuu wa Mkoa
wa Geita Robart Gabriel alisema kupitia sekta ya madini kuna mabadiliko makubwa
ya maendeleo mkoani Geita ikiwa huduma mbali mbali za kijamii zinaboreshwa hasa
huduma za Afya, Elimu na masoko ya kisasa kwa ajili ya wananchi wa kipato cha
chini.
Nae Makamu wa Rais wa Mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) Simon Shayo alisema wamejipanga kuhudumia jamii kwa
kujenga soko la wajasiliamali hali ambayo itapandisha kipato kwa akinamama na
wametenga sh 5.5 bilioni kwa ajili ya huduma za kijamii likiwemo soko la
wajasiliamali na dhahabu.
Comments
Post a Comment