Mahakama ya
wilaya ya Bukombe mkoa wa Geita imemtia hatiani mkazi wa kijiji cha Nyakafulu
aliyekuwa mchimbaji wa madini ya dhahabu kijijini hapo Ruben Misanga (47) kwenda
kutumikia adhabu ya mika 30 jela baada ya kumkuta na hatia ya kubaka mtoto wakike
mwenye umri wa miaka (10) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya
msingi Nyakafulu.
Hakimu mkazi
wa mahakama ya wilaya ya Bukombe Mjuni Mchunguzi akisoma hukumu kwa mshtakiwa
alisema mshtakiwa alitenda kosa hilo la kubaka Septemba 8 mwaka 2019 muda ambao
haukujulikana nyumbani kwake akiishi na
mtoto huyo wa kike akiwa amemfanya mke wake.
Mchunguzi
alisema kutokana na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka haujaacha shaka,
mahakama inamtia hatiani mshtakiwa
kwenda jela miaka 30 ili liwe fudisho kwa watu wengine wenye tabia kama
hiyo.
Awali
mwendesha mashtaka wa polisi wilaya ya Mbogwe Rashid Kitabu aliiambia mahakama kuwa matukio ya unyanyasaji
kwa watoto wadogo wa kike migodini yamekisiri na yanazidi kuongezeka.
Kitabu
aliomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa huyo ili kukomesha unyanyasaji
na ukatili kwa watoto wakike migodini.
Mshtakiwa
alipewa nafasi ya kujitetea hakujitetea chochote ndipo mahakama ikaamulu
mshtakiwa kwenda jela miaka 30.
Comments
Post a Comment