Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana
Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin Salabaga Ndugu aliwataka Maafisa Watendaji kugawa vifaa vya
kunawia kwa wananchi hasa kwenye maeneo yenye msongamano wa watu wengi ili
kufikia malengo ya Mbunge Biteko ya kuungana
na wananchi na serikali kujikinga na ugonjwa wa COVID 19 ambao bado ni janga
la kidunia.
Wito huo ulitolewa na Mwenyekiti huyo wakati
akikabidhi vifaa toka kwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko
ambavyo ni ndoo 100 na mabeseni 100 kwa
watendaji wa kata.
“Nampongeza Mhe Biteko kwa hatua hiyo ya kuwajali wananchi
wa Bukombe katika mapambano dhidi ya Corona”Alisema Ndugu.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Vijana alitoa wito kwa wadau
mbalimbali kumuunga mkono Mbunge Biteko kwa jitihada alizozionyesha
|
Comments
Post a Comment