Umoja wa Vijana UVCCM Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita umewapongeza wadau wa
maendeleo Wilayani hapa kwa kuchangia ujenzi nyumba ya Katibu wa jumuiya hiyo.
Kauli hiyo ilitolewa na mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Bukombe Nelvin Salabaga wakati alipokuwa ametembelea ujenzi wa nyumba ya Katibu wa Jumuiya Umoja wa Vijana .
Salabaga
alisema ujenzi huo ulianzishwa na jumuiya hiyo Februari 17 mwaka huu na
wanatarajia kukamilisha Mei 2020 kwa kutumia nguvu za wadau na michango ya
vijana.
Katibu
wa Jumuiya ya Vijana UVCCM Wilaya ya Bukombe Philbert Ngemela alisema ujenzi
utakapo kamilika utamuondolea changamoto ya kutembea umbali mrefu anapo kuwa
anaenda kutekeleza majukumu yake.
Nae Mwenyekiti wa Kamati ya Ujenzi na Afisa Tawala Wilaya AlLy Mketo alisema wamepokea
michango mbali mbali toka kwa wadau zikiwemo tofari 2000 zenye thamani ya Tsh milioni
2 toka kwa Mbunge Jimbo la Bukombe Mhe, Doto Biteko.
Mketo
alitoa wito kwa wadau wa maendeleo kuendelea kuchagia ili kufanikisha
ukamilishaji wa ujenzi huo.
Comments
Post a Comment