Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, wametoa motisha ya vitambaa vya
kushona suti kwa walimu na wajumbe wa kamati ya shule ya msingi Uyovu iliyo
faulisha wanafunzi watatu bora wa shule za serikali kitaifa.
Akizungumza
katika baraza hilo Afisa Elimu Taaluma shule za msingi Wilaya ya Bukombe Kassim
Mussa alisema shule ya msingi Uyovu ni miongoni mwa shule za msingi za serikali
86 Wilayani Bukombe.
Mussa alitoa
wito kwa walimu na viongozi wa kamati za shule kuendelea kufanya vizuri kwa
kusimamia mikakati waliojiwekea.
Nae Afisa
Elimu shule za msingi Wilaya ya Bukombe Shadurack Kabanga alisema katika ufaulu
wa mwaka 2018/19 shule ya msingi Uyovu ilifanya vizuri kitaifa kutokana na hali
hiyo halmashauri imetoa motisha kwa walimu na kamati ya shule.
Aidha
Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya shule msingi Uyovu Emmanuel Mpandiko
alisema wamekuwa na ushirikiano mzuri na walimu hali ambayo imewafanya walimu kuwa
na hari ya kujituma katika ufundishaji .
Mkuu wa shule ya msingi Uyovu Sevelin Jegu alisema
nafasi walioshika mwaka 2019 ni haki yao kwani wamekuwa wakiweka kambi kila unapo
karibia mtihani wa taifa na kuongeza kuwa mwaka huu wanamikakati waliojiwekea ili
kuhakikisha wanafanya vizuri tena.
Kwa upande
wake Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe na Diwani wa Kata ya
Bulega Erick Kagoma aliwapongeza walimu wa shule ya msingi Uyovu na kuishukuru
idara ya Elimu Wilaya kwa kutoa motisha kwa walimu walioiheshimisha
halmashauri.
Comments
Post a Comment