Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya Bukombe mkoani Geita
imetoa mkopo wenye mashariti nafuu kwa
lengo la kuwa kwamua kiuchumi kuanzia
ngazi ya familia.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba
kwenye sherehe ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyofanyika kiwilaya katika
uwanja wa Mwenge kata ya Uyovu.
Nkumba alisema serikali itahakikisha inaendea kuimarisha kundi
la wanawake katika frusa za maendeleo ikiwa Tsh milioni 146.6 zimekopeshwa kwa
mashariti nafuu kwa wanawake 575 vikundi 75.
Alisema mwaka 2018/19
vikundi 35 wanawake 175 walikopeshwa Tsh milioni 62.2 na 2019/20 vikundi 40 ambavyo
vinawanufaika wanawake 400 walipewa Tsh milioni 84.6.
Miongoni mwa wanufaika
wa mikopo ya serikali Conjester Mwita alisema tangu aanze ujasiliamali kupitia
mikopo inayo tolewa na serikali kwa mashariti nafuu amefanya maendeleo kwa
kukuza kipato cha familia na kuinuka kiuchumi.
Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Bukombe Mariana Genya alisema
Januari mwaka huu hadi Machi vikundi 13 vinatarajia kupewa mkopo wa Tsh milioni
38.5 vimesha tembelewa na kukizi vigezo.
Wakati huo huo wanawake walishiriki shughuli za ujenzi vyumba
vya madarasa shule ya Sekondari Uyovu kwa kusomba mawe kwa mjibu wa Mkuu wa Shule hiyo Simon Mashauri
alisema mahitaji ya madarasa 24 yaliyopo 9 upungufu 15 ingawa kunahatua mbali
mbali za ujenzi vyumba vinne vya madarasa kwa nguvu za wananchi na Mkuu wa
Wilaya
Akitoa shukran kwa niaba ya wanawake wa Bukombe Mwenyekiti wa
Jukwaa la Wanawake wa Mkoa wa Geita Jazaa Komba alianza kwa kutoa shukrani za
dhati kwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Mashaka Biteko
kwa jinsi anavyo washika mkono wamama wajasiriamali.
“Mhe Biteko mbali na
kututafutia fedha serikalini bado anatoa fedha zake za mfukoni ili sisi wamama wa Bukombe tuinuke kiuchumi”.Alisema
Komba
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wila ya Bukombe Dionis Myinga kwa pamja wakishiriki
shughuli za ujenzi vyumba vya madarasa shule ya Sekondari Uyovu kwa kusomba mawe kwenye siku ya wanawake Duniani
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akiwa na baadhi ya wamama wakishiriki katika zoezi la upandaji miti Shule ya sekondari Uyovu.
Wamama wakishiriki katika zoezi la upandaji miti Shule ya sekondari Uyovu.
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akisoma lebo ya bidhaa iliandaliwa na Bafremi Enterprises ambao wanahusika na utengenezaji na uuzaji wa sabuni aina mbalimbali za kunawia mikono,kufulia,kudekia na kuondoa harara na epele pamoja na ushonaji wa masweta na mazuria
Mama Angel Decoration ambae ni mtengenezaji wa keki na mapambo akimuonyesha Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba namna ya utengeneji wa vitu hivyo
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wila ya Bukombe Dionis Myinga wakiwa viongozi mbalimbali wa chama na serikali wakiwa kwenye banda la mama mjasiriamali anaejihusisha na utengenezaji wa Chaki(Bukombe Chalk)
Diwani wa Kata ya Bukombe Mhe Rozalia Msokola akizungumza kwenye sherehe ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyofanyika kiwilaya katika uwanja wa Mwenge kata ya Uyovu.
Diwani Viti maalum Tarafa ya Siloka Mhe Elizabeth Ngasa akizungumza kwenye sherehe ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyofanyika kiwilaya katika uwanja wa Mwenge kata ya Uyovu.
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wila ya Bukombe Dionis Myinga kwa pamja wakishiriki
shughuli za ujenzi vyumba vya madarasa shule ya Sekondari Uyovu kwa kusomba mawe kwenye siku ya wanawake Duniani
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akiwa na baadhi ya wamama wakishiriki katika zoezi la upandaji miti Shule ya sekondari Uyovu.
Wamama wakishiriki katika zoezi la upandaji miti Shule ya sekondari Uyovu.
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akisoma lebo ya bidhaa iliandaliwa na Bafremi Enterprises ambao wanahusika na utengenezaji na uuzaji wa sabuni aina mbalimbali za kunawia mikono,kufulia,kudekia na kuondoa harara na epele pamoja na ushonaji wa masweta na mazuria
Mama Angel Decoration ambae ni mtengenezaji wa keki na mapambo akimuonyesha Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba namna ya utengeneji wa vitu hivyo
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wila ya Bukombe Dionis Myinga wakiwa viongozi mbalimbali wa chama na serikali wakiwa kwenye banda la mama mjasiriamali anaejihusisha na utengenezaji wa Chaki(Bukombe Chalk)
Diwani wa Kata ya Bukombe Mhe Rozalia Msokola akizungumza kwenye sherehe ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyofanyika kiwilaya katika uwanja wa Mwenge kata ya Uyovu.
Diwani Viti maalum Tarafa ya Siloka Mhe Elizabeth Ngasa akizungumza kwenye sherehe ya maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani iliyofanyika kiwilaya katika uwanja wa Mwenge kata ya Uyovu.
Comments
Post a Comment