Radi yauwa ng’ombe 26 Kitongoji cha Sigoba Kata ya
Runzewe Mashariki Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita, wamekufa kwa kupigwa radi
wakati wakipata malisho hapo kijijini.
Afisa Mtedaji wa Kijiji cha Msonga Andrew Tungu aliwataja wamiliki
wa ng’ombe zilizo pigwa radi na kufa
papo hapo Bundala Saliboko
ng’ombe sita Joseph Mhangwa ng’ombe
sita Shikome Mlekwa ng’ombe sita Christopher Aloyce ng’ombe wanne Cecilia Sengerema ng’ombe watatu Ndaki Paul ng’ombe
mmoja wote wakazi wa kijiji cha Msonga.
Nae Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba wakati akitoa pole kwa niaba ya serikali kwa wafugaji aliwataka kuwa wavumilivu na kuto ingiza imani za
kishirikina kwani radi hupiga vitu mbali mbali zikiwemo nyumba hata binadamu.
Nkumba alitoa wito kwa waganga wa tiba asilia kutokuwa nyuma
ya hili kwa kupiga ramri choganishi kwa wafugaji na kusababisha uhasama kwa jamii .
Kwa upande wao wafugaji
Sengerema alisema ni mipango ya mungu radi kuuwa ng’ombe huku Mhangwa akiongeza kuwa
hawawezi kuingiza imani za kishirikina ingawa kila mtu anamtazamo wake.
Comments
Post a Comment