Mkuu wa wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Said Nkumba akiwahutubia
wajumbe wa kamati za maendeleo tarafa ya Siloka inayoundwa na kata tano.
wajumbe wa kamati za maendeleo tarafa ya Siloka inayoundwa na kata tano.
Katibu tawala wa wilaya ya Bukombe Paul Cheyo akitambulisha safu aliyoambatana nayo
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, Said Nkumba amewaonya
baadhi ya watumishi wa Serikali wanaokwamisha
miradi ya maendeleo kukamilika kwa wakati iliyoibuliwa na wananchi kwa muda
mrefu.
Nkumba aliyasema hayo kwenye kikao cha kazi kilichokuwa
kimejumuisha wajumbe wa kamati za maendeleo tarafa ya Siloka inayoundwa na
kata tano.
Nkumba alianza kwa kupongeza watumishi wanaofanya vizuri
katika kusimamia miradi kisha kuwageukia ambao hawashiriki kikamirifu na kukwamisha
miradi hiyo kukamirika.
Nkumba alitoa wito kwa wenyeviti wa vitongoji na vijiji
kushirikina na maafisa watendaji wa vijiji na kata ili kuhakikisha miradi
inakamilika na kuwashirikisha wananchi ili wanufaike na fedha ambazo zinaletwa na
serikali walioiweka madarakani.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Bukombe Dioniz Myinga
aliwasihi maafisa watendaji wa kata kugawa madarasa kwenye vitongoji ili
wachange na kukamirisha ujenzi.
Myinga aliwaomba kusimamia michango ya wananchi kikamirifu na kuwa
wawazi juu ya makusanyo ya fedha ambazo zimekusanywa ikiwemo kuzingatia
muda waliojiwekea.
Comments
Post a Comment