WANANCHI WA CHAGISHANA KUJENGA SHULE


Mbunge wa jimbo la Bukombe Doto Biteko akihutubia kwenye mkutano wa hadhara kijiji cha Bulama

Katibu wa itikadi na uenezi CCM wilaya ya Bukombe  Ladislaus Soku akimpongeza Mhe. Biteko kwanamna anavyochangia maendeleo kwa wananchi 
 

Muonekano wa jengo la shule ya msingi Bulama Baada ya nguvu za wananchi na wadau mali mbali wa elimu akiwemo Mbunge wa jimbo la bukombe Mhe. Doto Biteko


 Wananchi wa kijiji cha Bulama kata ya Runzewe mashariki wilaya ya Bukombe mkoani Geita, wameanza kuchagishana sh 1500 kila mtu Mwenye uwezo wa kufanya kazi ili kukamilisha ujezi wa shule ya msingi Bulama.

Afisa mtendaji wa kijiji cha Bulama Andrew Mbikilwa  alisema wananchi walianza kujichagisha sh 1500 kila mtu wenye uwezo wa kufanya kazi Novemba 2017 mradi utakamilika Desemba 2020. 

Mbikilwa alisema mradi huo hadi kukamilika madarasa matatu na ofisi moja itagharimu sh 12.7 milioni  wananchi wamesha changia sh 10.6 milioni wadau wa maendeleo wametoa sh 6000 na ujenzi uko hatua ya lenta kwa thamani ya sh 11.2 milioni. 


Mbunge wa jimbo la Bukombe Doto Biteko akiwa  kijiji cha Bulama alipokwenda ziara kuhamasisha maendeleo aliwaunga mkono wananchi mifuko 160 ya saruji na mabati pamoja na misumari

Biteko alitoa wito kwa viongozi wa serikali kuacha kutumia nguvu nyingi kukusanya michango kwa wananchi ikiwa wengine wanajitolea nguvu zao kwa kusogeza mchanga, mawe, maji wengine wanachagia mali zao.

Nae Mkazi wa kijiji cha Bulama Siphania Daniel alisema kupitia mchango wa Mbunge Biteko amewahamasisha kuchagia ili mradi huo ukamilike ambao utaondoa adha ya kutembea umbali mrefu kwenda Kufuata elimu.

Comments