Wadau wa kupambana na maambikizi ya Ukimwi wakiwa kwenye warsha ya kudhibiti UKIMWI iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko kwa kushirikiana na shirika la International Control Aids Program I.C.A.P.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko akiwataka wanawake kuendelea kuelimisha jamii juu ya maambukuzi ya virusi vya ukimwi
Afisa Tawala wa Wilaya ya Bukombe Ally Mketo wakati akifungua warsha ya kudhibiti UKIMWI iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko kwa kushirikiana na shirika la International Control Aids Program I.C.A.P.
Wanawake Wilayani Bukombe wakipewa mafunzo ya kudhibiti UKIMWI
Wanawake Wilayani Bukombe Mkoa wa Geita wameaswa kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya maambukizi ya Ukimwi .
Aliyasema hayo Afisa Tawala wa Wilaya ya Bukombe Ally Mketo
wakati akifungua warsha ya kudhibiti UKIMWI iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la
Bukombe Doto Biteko kwa kushirikiana na shirika la International Control Aids
Program I.C.A.P.
“Takwimu za mwaka 2019 watu waliopima na kukutwa na
maambukizi ni 2576 ikiwa wengi wao ni wanawake ambao ni 1678 na wanaume 897 hali ambayo ina pelekea
kuwa hali ya maambukizi kufikia asilimia 5.3 wilayani hapa”.Alisema Mketo
Nae Mratibu wa Shirika I.C.A.P. Mkoa wa Geita Mwedi Mohamed
alisema wametoa mafunzo ya kujikinga na UKIMWI kwa watu 250 Wilaya ya Bukombe ikiwa
lengo la utowaji wa Elimu hiyo ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 asilimia 95 ya watanzania wawe
wanajua hali zao, na asilimia 95 wawe wameuganishwa kwenye huduma ya dawa, huku
asilimia 95 wawe wamefubaza UKIMWI.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko alimuomba Mkurugenzi Mkuu wa shirika la
International Control Aids Program I.C.A.P linalo toa Elimu kwa makundi mbali
mbali ili kuepuka na maambukizi ya UKIMWI Tanzania Dk Fernado Morales kuendelea
kuwaelimisha wanawake kupima na kujikinga na maabukizi.
Comments
Post a Comment