WACHUNGAJI 11 WAWEKEWA WAKFU RASMI

Afisa Tawala Wilaya ya Bukombe Ally Mketo akizungumza na waumini wa Kanisa la Ufunuo jimbo la Geita lililopo mjini Ushirombo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba. 

Diwani wa Kata ya Igulwa Mhe. Richard Mabenga akizungumza na waumini wa Kanisa la Ufunuo jimbo la Geita lililopo Ushirombo mjini. 


  Askofu wa kanisa la Ufunuo jimbo la Geita, Heryyabwana Majebele akiwapaka mafuta ya utumishi wachungaji wasimikwa.


 Mkuu wa Chuo cha Biblia Geita Bible Training Center (GBTC) Alexander Maningu akiwavisha kola Wachungaji 11 baada ya kuwekwa wakfu.




Wachungaji 11 wawekewa wakfu na Askofu wa Kanisa la Ufunuo Jimbo la Geita, Heryyabwana Majebele baada ya kuhitimu masomo yao chuo cha Biblia Geita Bible Training Center (GBTC) na kufikia daraja la uchungaji.

Askofu Majebele akiwaweka wakfu wachungaji wapya 11 aliwataka kuacha tamaa za kidunia na kufanya kazi  waliyoitiwa na Mungu kwa kuwa mfano wa kuigwa ndani ya makanisa  watakayo pewa na jamii inayo wazunguka.

“Wachungaji watano niliwavua nyadhifa baada ya kupata taarifa zisizo mpendeza Mungu kutoka kwa waumini wa makanisa nikawaita na kuwauliza juu ya fununu hizo wakakili makosa, sasa na wachungaji ambao nawateuwa mjipange mkitenda dhambi nitawatumbua zingatieni maadili ya kiutumishi kama mlivyo fundishwa chuoni” alisema Askofu Majebele.

Kwa upande wake Afisa Tawala wa Wilaya ya Bukombe Ally Mketo alimpongeza Askofu Majebele kwa hatua aliyoichukuwa dhidi ya watumishi hao waliopotokwa na kusisitiza kuwa  asingelikua hachukii dhambi angeliwafumbia macho wachungaji hao wanao kiuka maadili ya ki Mungu.

Mketo alimuomba Askofu Majebele kuendelea na msimamo wake katika kutekeleza majukumu ya kusimamia kanisa na kushirikiana na serikali kwa kuchagia maendeleo kikamilifu.

Miongoni mwa wachugaji waliowekewa wakfu Zawadi Jemes alisema hakutarajia kama angepata uchungaji baada ya kuhitimu masomo lakini nimpango wa mungu kumteuwa.

Jemes alisema atahakikisha anamtumikia Mungu kikamilifu kwa kuokoa roho zilizo potea popote atakapo tumwa na Askofu Majebele.




Comments