RC GEITA AAZISHA KAMPENI YA KUMALIZA UPUNGUFU WA MADARASA



Mkuu wa Mkoa wa Geita Robart Gabriel  akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba wakishirikiana na wananchi wa Kata ya Katente kusomba mawe baada ya kuchimba msingi.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Robart Gabriel  akiwa amebeba jiwe na mkazi wa Kata ya Katente wakati wa kujitolea kujenga madarasa shule ya sekondari Katente .


Wakazi wa Kata ya Katente wakati wa kujitolea kujenga madarasa shule ya sekondari Katente  na aliye beba jiwe ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Bukombe Dionis Myinga akishiriki.




Mkuu wa Mkoa wa Geita Robart Gabriel ametoa wito kwa wadau wa elimu na maendeleo Mkoani hapa kuchangia mali zao kwa kuwashika mkono wananchi kwenye miradi ya ujenzi wa Zahanati, Vituo vya Afya na  madarasa shule za msingi na sekondari.

Gabriel alitoa wito huo wakati wauzinduzi wa kampeni ya kumaliza upungufu wa madarasa shule za msingi na sekondari mkoani hapa uzinduzi ikiwa uzinduzi huo ulifanyika shule ya sekondari katente ilioko Wilaya ya Bukombe kwa kushirikiana na wananchi kuchimba msingi na kusomba mawe ili kumaliza upungufu wa madarasa 16 shuleni hapo.

“Kampeni hii haita ishia Wilaya ya Bukombe bali ni Wilaya zote za Mkoa wa Geita, wahakikishe wana anzisha ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za msingi na sekondari ili serikali ya Mkoa itafute fedha za ukamilishaji wa  vyumba vya madarasa vitakavyo jengwa kwa nguvu za wananchi” alisema Gabriel.

Na kupitia uzinduzi huo wa kampeni ya kumaliza changamoto ya upungufu wa madarasa kimkoa Mkuu wa Mkoa Gabriel alikusanya mifuko 200 kati ya  mifuko hiyo 50 ilitolewa na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko.

Mkazi wa Kata ya Katente Edward Samson alisema wameaza kushiriki kuchimba msingi na kusogeza mawe kutokana na Mkuu wa Mkoa wa Geita Robart Gabriel kufika na kuonyesha hamasa kubwa kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba.

Nae Afisa Taluma shule za sekondari mkoa wa Geita Christabela Ngatoluwa alisema shule za sekondari kwa mkoa wa Geita zipo 118 huku shule za sekondari kidato cha tano na sita zipo  2.

Ngatoluwa alisema mahitaji ya vyumba vya madarasa ni 615 madarasa yaliyopo 398 upungufu madarasa 217 na kwamba upungufu huo kitaluma ni changamoto kwa wanafunzi inasababisha msongamono hali ambayo inawafanya wanafunzi kutofanya vizuri kitaluma.

Mkuu wa shule ya katente sekondari Sigano Mokiri alisema shule inawanafunzi 1530 wasichana 731 wavulanaa 799 uhitaji wa madarasa 34 yaliyopo 18 upungufu 16 alisema kupitia hamasa ya serkali ya mkoa na wilaya wananchi wamehamasika kujitolea kuchimba msingi  vyumba vyote ambavyo ni mapungufu ili ujenzi uanze.

Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba alisema kutokana na moto uliowashwa na Mkuu wa Mkoa Wilayani Bukombe ni kwa nia ya dhati kuleta maendeleo.

Nkumba aliwaomba wananchi kuendelea kujitoa nguvu zao kwa kuchimba msingi ya madarasa na miradi mingine ikiwemo kusogeza mawe na mchanga, na maji ili serikali inapoleta fedha zikamilishe mradi na fedha zibaki na kuazisha miradi minginge.


Comments