DC NKUMBA AWATAKA WALIOSHIKA NAFASI YA SERIKALI ZA MITAA KUHAMASISHA MAENDELEO

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Kata ya Iyogelo.

Diwani wa Kata ya Iyogelo Juma Lushiku akipeana mkono na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Wilaya ya Bukombe Ladslous Soku baada ya kusoma utekelezaji wa Ilani ya CCM Kata ya Iyogelo.


Diwani wa Kata ya Iyogelo Juma Lushiku akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Kata ya Iyogelo.


Diwani wa Kata ya Iyogelo  akikabidhi taarifa ya utekelezaji kwa  Juma Lushiku Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe ambae pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo Said Nkumba.  



Diwani wa Viti maalumu Rahel Sololo akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Kata ya Iyogelo.





Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe ambae pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo Said Nkumba amewataka wenyeviti wa vitongoji na vijiji kuhamasisha wananchi kushiriki kikamirifu kwenye miradi ya maendeleo.

Nkumba aliyasema hayo wakati akihutubia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Kata ya Iyogelo .

Pia Nkumba alisema wasimamie utekelezaji wa ilani kwa mtu mmoja mmoja kwa kuinua uchumi wao kupitia kilimo cha kisasa na kuachana na kilimo cha mazoea kisicho na tija .

Awali Diwani wa Kata ya Iyogelo Juma Lushiku wakati akiwasilisha utekelezaji wa ilani alianza kwa kumshukuru Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko kwa mchango wake mkubwa wa hali na mali katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.

“Nawaomba viongozi wa vitongoji na vijiji wa muda uliopita bila kujali itikadi ya kisiasa nao wawe chachu ya kuhamasisha wananchi wahakikishe kuwa wanashiriki kwenye miradi ya maendeleo”Alisema Lushiku.

Lushiku alisema kuna miradi 26 yenye thamani ya Tsh bilioni 1.8 iliyotekelezwa ndani ya kata hiyo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa shule ya sekondari Busonge uliogharimu Tsh milioni 33,miundo mbinu ya madarasa shule ya msingi Bugando,kliniki za baba,mama na mtoto kwenye Zahanati mbili na miundo mbinu ya umeme na barabara.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kata Mwanjia Said alisema ili kufikia malengo ya maendeleo katika uboreshaji wa miundombinu ya madarasana majengo ya kutolea huduma za Afya wanasiasa washirikiane ili kuhamasisha wananchi kushiriki kwenye miradi kwa kuchagia nguvu na mali.

Nae Afisa Kilimo wa Kata hiyo Asteria Kibasa aliwaomba viongozi walio chaguliwa hivi karibuni serikali za mitaa uhamasisha wakulima kulima mazao ya chakula na biashara kwa kufuata ushauri wa watalamu ili waondokane na kilimo cha mazoea na kulima kilimo cha faida ili waweweze kufanikiwa kukuza uchumi wa familia na taifa kwa ujumla.


Comments