TAKUKURU YAKUTANISHA WADAU WA SEKTA YA ELIMU KUJADILIANA JUU YA FEDHA ZA ELIMU BURE.






Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita  imekutana na wadau wa elimu na kutoa elimu juu ya  fedha zinazotolewa na serikali kila mwezi kutekeleza Elimu bure.
Afisa wa TAKUKURU Wilaya ya Bukombe toka dawati la utafiti na uchunguzi Bosco Mwidadi alisema robo ya mwaka wafedha 2018/19 TAKUKURU walifanya ufatiliaji kwenye miradi ya maendeleo hasa katika mpango wa fedha zinazotolewa na serikali kutekeleza Elimu bure katika shule 10 kati ya shule zamsingi 79.
 Mwidadi alisema hayo kwenye warsha  ya wadau wa Elimu katika ukumbi wa mikutano halmashauri ya Wilaya kilichohudhuliwa na wenyeviti wa kamati ya maendeleo ya shule na walimu wakuu wa shule za msingi 79 na Maafisa Elimu kata 17 madiwani na wananchi, ili kujadili matokeo ya TAKUKURU waliyo ya baini kweye ufatiliaji wa miradi ya maendeleo mashuleni.
“ TAKUKURU iligudua ukeukwaji wa maelekezo ya serikali kwenye fedha za Elimu bure”. Alisema Mwidadi
Aliongeza kuwa fedha zinatumika bila kufuata mwongozo kuwa asilimia 30, ukarabati asilimia 30 zinunua vifaa vya kujifunzia na kufundishia, asilimia 20 itumike kwa ajili ya mitihani asilimia 10 kwa ajili ya utawala asilimia 10 itumike kwa ajili ya michezo.
Mwidadi alisema  fedha za michezo zinatumika kwa wingi  na za kugharamia mtihani wa moko na ukarabati, pia upande wa manunuzi kuna shida kubwa kwani kunaukeukwaji wa sheria za manunuzi ikiwa ni pamoja na kumbu kumbu za manunuzi na malipo hazitunzwi  hali ambayo inasababisha shule kushindwa kumudu gharama za kujiendesha.
Alisema kabla ya TAKUKURU kuanza kuchukuwa hatua wameona wawaite na kuwakumbusha kutunza kumbu kumbu za manunuzi na malipo.
Nae Mwenyekiti wa Walimu Wakuu Wilaya ya Bukombe Charles Kisombi alisema ni kweli kunachangamoto kubwa katika utekelezaji wa fedha za Elimu bure .
Kisombi alisema walimu wengi walikuwa hawazingatii miongozo za manunuzi na malipo wakijua wako sahihi kumbe wako nje ya taratibu kutokana na TAKUKURU kuwapa mafunzo walimu wameyapokea kwa njia chanya.
Kisombi alitoa wito kwa walimu wakuu kuzingatia sheria za manunuzi na malipo kupitia mafunzo hayo ya TAKUKURU na kwamba walimu wakuu wanamikakati ya kuita watalamu ili wafundishwa mifumo na sheria za manunuzi na malipo katika utekelezaji wa Elimu bure.
Kwa pande wake Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akitoa taarifa ya fedha zinazo tolewa na serikali kila mwezi kutekeleza Elimu alisema serikali tangu 2015 hadi septemba mwaka 2019 Tsh bilioni 2.12 zimepokelewa kwa ajili ya Elimu bure shule 79 za msingi.
 MWISHO

Comments