MHE. BITEKO AACHA NEEMA UJENZI WA ZAHANATI IMALANGUZU.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko na Waziri wa Madini amehiriki  kukamirisha mradi wa ujezi wa zahanati iliyo anza kujengwa kwa nguvu za wananchi 2015.

Biteko alibainisha kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya mabati 250,mbao za kupaulia zahanati hiyo 
“Wananchi wanaoanzisha miradi ya maendeleo lazima aniwaunge mkono pale wanapofikia ili kusogeza huduma kwa wananchi”.Alisema Biteko

Wakati huohuo Biteko alitoa mifuko mia moja  kwa ajili ya ujenzi wa choo cha wanafunzi katika shule ya msingi Imalanguzu na kuwaomba wananchi kuendelea kushirikiana na serikali kwa kuibuwa miradi ya mandeleo kwa kuazisha ujezi ili wadau wa maendeleo wachangie mali zao.

Awali Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Imalanguzu Kata ya Bukombe Yusuph Maige alisema Kijiji kina Kitongoji sita watu kwa mjibu wa sense 2012 kijiji kina watu 2491.

 Maige alisema kutokana na kutokuwepo huduma za Afya wananchi waliazicha ujenzi wa Zahanati mwaka 2015 na kuchangia sh 38 milioni na hadi kukamilika mradi huo mwaka 2021 utagharimu sh 100 milioni.

Nae Diwani wa Kata ya Bukombe Rozalia Masokola alimshukuru Mbunge Biteko kwa msaada wake nakuwasihi wananchi kuendelea kumuunga mkono anapohamasisha maendeleo.


Comments