MHE BITEKO ASHIRIKI IBADA YA MAOMBEZI YA WATOTO


 Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Mashaka Biteko amewataka wazazi na walezi kuwalea watoto wao kwa kuzingatia maadili mazuri ili kuwa na jamii bora.

Biteko alitoa wito huo kwenye ibada ya kubariki watoto chini ya miaka mitano katika Kanisa la E.A.G.T (Kanani) Uyovu Kata ya Uyovu Tarafa ya Siloka Wilayani Bukombe.

Biteko alisema wajibu wa mzazi ni kulea mtoto katika misingi ya  maadili mema ikiwa ni pamoja na kuwapa elimu na kuongeza kuwa  watoto walio na madili mazuri serikali itapunguza changamoto za vijana  kujihusisha na vitendo vinavyopelekea uvunjaji wa sheria.
Katika ibada hiyo Mbunge Biteko  aliwaomba wananchi kushirikiana na viongozi wa serikali za mitaa waliopatikana kwenye uchaguzi uliofanyika Novemba 24 mwaka huu.



Kwa upande wake Mchungaji wa Kanisa la E.A.G. T (Kanani) Uyovu Yusuph Kinoja wakati akibariki watoto alisema maombi ya Baraka kwa watoto chini ya miaka mitano yanawafanya watoto hao kukuwa katika maisha ya duniani kwa hekima,busara  pamoja  na maadili ya Kimungu .

Kinoja alimshukuru Mbunge Biteko kwa kufika kanisani hapo kushiriki ibada na kwa namna alivyo shiriki kutoa mchango wa ujenzi wa kanisa sambamba na ununuzi wa gari la mchungaj wa kanisa hilo.

Comments