WADAU WATAKIWA KUTOA MALI ZAO KWENYE MIUNDOMBINU YA SHULE


 Shule ya Msingi Ibambilo baada ya kuezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua. 


 Mwonekano wa Shule ya Msingi Ibambilo baada ya kuezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua. 


Hali halisi ya  choo cha  wanafunzi wa kike baada kuezuliwa.


  Picha ya Kanisa la Wadventista Wasabato Bulega baada ya kuezuliwa.



Diwani wa Kata ya Bulega  Tarafa ya Ushirombo Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, Erick Kagoma amewaomba wadau wa maendeleo kushirikiana  na wananchi wa Kata hiyo kuongeza nguvu za haraka  kwenye ujenzi wa miundo mbinu ya madarasa ya shule ya msingi Ibambilo baada ya kuezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua. 

Erick aliyasema hayo wakati akizungumza na mwananchi shuleni hapo alipofika kujionea hali ya uharibifu wa shule hiyo na baada ya nyumba za ibada  ikiwemo kanisa la waadventista Wasabato na kuwasihi wananchi hao kuanza kujenga nyumba zenye ubora kwa kuziwekea renta

Mkuu wa Shule ya Msingi Ibambilo Magembe Shimba alisema tukio lilitokea Oktoba 1 majira ya saa 9:00 mwaka huu kabla ya wanafunzi kutawanyika.

Shimba alisema mvua hiyo iliyoambatana na upepo mkali  ilianza na kuharibu miundombinu ya vyumba vya madarasa vinne na choo cha  wanafunzi wa kike.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko aliwapa pole wanafunzi na walimu kwa kunusurika na tukio hilo wakati huo huo alikabidhi msaada wa Tsh milioni 1 wakati halmashauri inajipanga kuweka bajeti ya ukamilishaji wa miundombinu ya shule hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba alitoa wito kwa wananchi wa Bukombe kuwa makini na msimu wa mvua sambamba na kujenga tabia ya kuitunza miti ya uoto wa asili inayo saidia majanga ya upepo.

Nkumba amewaagiza watalamu wa halmashauri kufanya haraka kufanya tathimini ya gharama zitakazo tumika ili kuhakikisha miundo inakamilika kwa wakati.

Nkumba alitoa wito kwa wananchi kuboresha nyumba zao hasa kuondokana na kuegeshea mabati mawe na magogojuu ya nyumba  hali ambayo ni hatari kwa wakati wa mvua ambazo zinanyesha kwa kuambatana na upepo mkali.

Comments