KATIBU MWENEZI CCM-BUKOMBE ASEMA JUU YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

 Wakugombea nafasi za uenyekiti wa vitongoji kutoka Kata ya Katente kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi wakiwa wamefika kwa
Mkurugenzi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Katentekwa ajili ya uchukuaji wa fomu.

Mkurugenzi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Katente Issa  Shaaban akitoa maelekezo kwa wagombea waliofika kuchukua fomu za kugombea nafasi za uenyekiti wa vitongoji kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
 
 
Wakugombea nafasi za uenyekiti wa vitongoji kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi wakiwa katika Ofisi ya chama chao kwa ajili ya zoezi la kujaza fomu za kugombea. 
 
Mgombea uenyekiti kitongoji cha majengo Elizabeth Mwenda akirejesha fomu ya kugombea nafasi ya uenyekiti
 Mgombea uenyekiti ktongoji cha bomani Ndugu Bundala Ngavune akirudisha fomu kwa msimamizi msaidi wa uchaguzi kata ya katente
 Mgombea uenyekiti kitongoji cha kitangili Cosmas Pobobo Machibya akitoa mkono wa shukrani kwa Mkurugenzi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Katente Issa  Shaaban kwa  niaba ya wenzake

Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Wilaya ya Bukombe Ladislaus Soku  alisema Wilaya ya Bukombe ina vitongoji 348 vijiji  vya uchaguzi 64 Kata 17 Tarafa tatu na kuwahakikishia ushindi wa gombea kupitia CCM  baada ya kujipanga na uchaguzi  kikamilifu kwa asilimia  99 wanauhakika wa ushindi vitongoji na vijiji vyote.
Nae Katibu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Kata ya Katente Eligius Nyabwisho alisema Kata ina mitaa mitano wagombea wako watano na kwamba CCM imejipanga kuhakikisha wagombea wanashinda.
Mgombea Kitongoji cha Majengo Elizabeti Mwenda alisema kazi aliyo nayo ni kutetea kiti chake kwa wananchi kwani tangu 2014 alishinda na kwamba Chama Cha Mapinduzi CCM kimemwamini tena.
“Wananchi waliniamini na sasa wananiamini nitashinda”Alisema Mama Mwenda.
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Uchaguzi Kata ya Katente Issa  Shaaban alisema Kata ina vitongoji vitano na wamefika wagombea watano kuchukuwa fomu  na kurudisha saa 6:20 mchana huku wagombea watano kwa tiketi ya Chadema wamefika na kuchukuwa fomu lakini hawaja rudisha.
Shaban alisema wanategemea wagombea kuja kuchukuwa fomu toka vyama vya siasa vinne CCM, CHADEMA, CUF, ACT wazalendo na mwisho wa kuchukuwa fomu na kurudisha ni Novemba 7 mwaka 2019.
Shaban alitoa wito kwa wagombea na viongozi wa vyama vya siasa kufuata  sheria,kanuni na miongozo iliyotolewa na tume ya uchaguzi kupitia mkurugenzi wa uchaguzi ngazi ya Wilaya alieteuliwa na Waziri mwenye dhamana ili kamati za madili zisipate kazi sana katika uchaguzi wa serikali za mitaa 2019.
    
 
 

Comments