WAZIRI WA NISHATI AMSIMAMISHA KAZI MENEJA WA TANESCO - BUKOMBE

 
 




Waziri wa Nishati Dk Medard Kareman amemsimamisha kazi Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, Thadey Mapunda kwa kutoridhishwa na utendaji kazi wake kwa kushindwa kusambaza nguzo na kuwasha umeme wa Rea awamu ya tatu kwa wakati na kutoza wananchi fedha za nguzo kinyume na maelekezo ya  serikali ya mwananchi kununua nguzo za umeme.
 
Dk Karemani alimsimamisha kazi meneja huyo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika uwanja wa Kapela Kata ya Igulwa Wilayani hapa baada ya Waziri kupitia maeneo ya stendi ya mabasi kukuta hakuna umeme na kutoka mjini Ushirombo kwenda mtaa wa Magorofani nguzo zimechimbiwa jana huku meneja akimdanganya kuwa nguzo hizo zina zaidi ya mwezi zimesimama.

“Nimekuja Bukombe mara tatu na kutoa maagizo lakini bado kuna malalamiko makubwa kwa wananchi wanataka umeme, sasa ifikie mwisho maana kabla ya kufika hapa kiwanjani nimefanya ukaguzi mdogo nimepita soko kuu na stendi ya mabasi hakuna umeme wakati ni swala la kutatuliwa siku moja.
                   "Nimetoa maelekezo kesho septemba 15 iwekwe transfoma ili umeme uanze kuwaka na nimeenda mtaa wa kapela kuna nyumba nzuri lakini hazina umeme nifedheha kubwa sana harafu namuuliza Meneja nguzo amechimbia lini ananijibu mwezi jana huku zinaonekana amechimbia jana au leo asubuhi baada ya kusikia nakuja sijalidhishwa na utendaji kazi wa meneja tanesco Wilaya na naangiza kuanzia sasa namsimamisha kazi asionekane hata kwenye msafara wangu na kesho meneja wa Mkoa leta Meneja mwingine hapa hakuna mwananchi kutozwa zaidi ya sh 27000 na hakuna kununua nguzo kama kuna Meneja anauza nguzo ajifute kazi”alisema Dk Karemani.

Dk Karemani alitowa maelekezo kwa Meneja wa Tanesco Mkoa wa Geita Joachim Ruweta na Mkandaras wa Mradi Bakari Abdallah kwa kushirikiana na Meneja wa Kanda Maclean Mbonile siku 30 mradi uwe umefika kijiji cha  Nipha, Majengo,Kelezia, Magorofani,stendi kuu ya mabasi pamoja na maeneo mengine ambayo hayajafikiwa na umeme.
 
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akitoa taarifa ya mradi wa Rea awamu ya tatu alisema mradi huo utafika kwenye vitongoji 348 na vijiji 70 vya kiumeme ndani ya kata 17 na unatekelezwa na mkandarasi aitwaye whitecityguangdong jv ltd mradi ulianza kutekelezwa wilayani hapa Januari 2018  na utakamilika mwaka 2020  utagarimu sh14.8 bilioni wateja wapatao 406 wamesha unganishiwa umeme na nguzo zimefikishwa kilomita 196 kati ya hizo nguzo kilomita 31.20 waya umevutwa.


Mbunge wa Jimbo la Bukombe Doto Biteko alisema iwapo umeme utafika kwa wananchi kwa wakati itawafanya kuwa na fursa za kujiajiri na kupandisha uchumi wa familia zao na Taifa.

Biteko alisema kuna vijiji ambavyo vilishasahaulika viko Kata ya Uyovu ikiwemo Kijiji cha Kanembwa na kumuomba Waziri wa Nishati kuona umuhimu wa kufikisha mradi huo ili wananchi wafanye kazi za uzalishaji mali kwa kuanzisha viwanda vidogovidogo katika maeneo yao.


Mkandaras wa mradi huo toka kampuni ya whitecityguangdong jv ltd Baraka Abdallah  alimuhakikishia Waziri wa Nishati kuwa ifikapo Desemba mwaka huu atakuwa amekamirisha Mradi.





Comments