Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin
Salabaga akuzungumza na wanafunzi ambao ni wanamichezo wa Shule ya Sekondari Runzewe.

Katibu Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Philibert Ngemela akitoa salamu kwa vijana wanamichezo wa Shule ya Sekondari Runzewe (hawapo pichani).

Katibu wa Hamasa na Chipukizi Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Johari Kivia akitoa nasaha kwa vijana wanamichezo wa Shule ya Sekondari Runzewe (hawapo pichani).
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin Salabaga akimkabidhi jezi nahodha wa timu ya Shule ya Sekondari Runzewe.
Uongozi wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe,wajumbe wa baraza hilo wakiwa na wanafunzi ambao ni wanamichezo wa Shule ya Sekondari Runzewe katika picha ya pamoja.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin Salabaga akimkabidhi jezi nahodha wa timu ya Shule ya Sekondari Uyovu.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin Salabaga akuzungumza na wajumbe wa baraza maalum la vijana Wilaya lililofanyika katika Ofisi za CCM Kata ya Uyovu.

Mkuu wa Wilaya Bukombe Said Nkumba akizungumza na Wajumbe wa Baraza maalum la Vijana Wilaya ya Bukombe.

Katibu Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Philibert Ngemela akitoa salamu kwa vijana wanamichezo wa Shule ya Sekondari Runzewe (hawapo pichani).

Katibu wa Hamasa na Chipukizi Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Johari Kivia akitoa nasaha kwa vijana wanamichezo wa Shule ya Sekondari Runzewe (hawapo pichani).
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin Salabaga akimkabidhi jezi nahodha wa timu ya Shule ya Sekondari Runzewe.
Uongozi wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe,wajumbe wa baraza hilo wakiwa na wanafunzi ambao ni wanamichezo wa Shule ya Sekondari Runzewe katika picha ya pamoja.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin Salabaga akimkabidhi jezi nahodha wa timu ya Shule ya Sekondari Uyovu.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin Salabaga akuzungumza na wajumbe wa baraza maalum la vijana Wilaya lililofanyika katika Ofisi za CCM Kata ya Uyovu.

Wajumbe wa Baraza maalum la Vijana
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Ccm Wilaya ya Bukombe Nelvin
Salabaga amewataka Vijana kuwa mstari wa mbele kuunda vikundi vya ujasiriamali ili kunufaika
na mikopo inayotolewa kwa vijana kila mwaka wa fedha na Halmashauri ya Wilaya ya
Bukombe.
Salabaga alitoa wito huo wakati akihutubia baraza la
vijana (Uvccm) lililofanyika Kata ya Uyovu Tarafa ya Siloka Wilayani hapa.
Alisema iwapo vijana watachangamkia fursa hiyo ya
mkopo na kuifanyia kazi kwenye miradi na sio kuzichezea fedha kwa kujiingiza
kwenye starehe wataweza kujikwamua kiuchumi kwa mtu mmojammoja na jamii nzima
kwa ujumla.
Katika ziara hiyo Salabaga alitembelea Shule ya
Sekondari ya Runzewe na Uyovu na kuzungumza na wanafunzi ambao ni wanamichezo wa
shule hizo na kuwakabidhi jezi za michezo zilizotoka kwenye Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko.
Awali Mwenyeti wa Jumuiya ya Vijana Ccm kata ya Uyovu
wakati akimkaribisha Mwenyekiti wa Wilaya alianza kwa kumpongeza kwa kazi anazozifanya za kuijenga jumuiya hiyo
na kuwafanya vijana kuwa wamoja.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya Bukombe Said Nkumba
aliwataka vijana kutokubeza wito wa Mwenyekiti wao wa Wilaya ili kunufaika na
Serikali.
Nkumba aliwataka Vijana kuchangamkia fursa ya kugombea
uongozi katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajia kufanyika mwaka huu na
kutokutumiwa vibaya na katika uchaguzi huo kwa maslahi ya mtu binafsi na
kusahau uzalendo wanchi.
Comments
Post a Comment