UWT BUKOMBE KUNUFAIKA NA ELIMU YA UJASIRIAMALI


Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Geita Mhe. Josephina Chagulla akizungumza na wajumbe wa Jumuiya ya wanawake Ccm Wilaya ya Bukombe
 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanawake Ccm Wilaya ya Bukombe Agnes Sayi akionyesha furaha za ujio wa Mbunge huyo na kufungua mkutano huo.


Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Geita Safia Bakari akizungumza na Jumuiya ya wanawake Ccm Wilaya ya Bukombe

Mkurugenzi wa Kampuni ya open mind and though organizasion (OMTO) Anna Haule akitoa somo la ujasiriamali.

Mmoja wa Wakufunzi akitoa mada kwa furaha kabisa.


Wajumbe wa UWT Wilaya ya Bukombe wakiwa katika mapokeo.







Jumuiya ya wanawake Ccm Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita imenufaika na elimu ya Ujasiriamali iliyotolewa na wakufunzi waliokuwa wameambatana na Mbunge wa Viti Maalum Mkoani hapa Josephina Chagulla 

Chagulla kabla ya kuwakaribisha watalamu wa mafunzo ya ujasiriamali kuzungumza na wamama hao alisema wanawake wajasiriamali Mkoani hapa wanamitaji lakini hawana utalamu wa kuongeza thamani ya bidhaa kwa kuweka kwenye vifungashio vilivyo katika ubora.

Alisema kupitia mafunzo hayo ambayo watayapata yatawasaidia kuwa wa bunifu na kuongeza thamani ya bidhaa na kuwahakikishia upande wa changamoto ya soko la bidhaa zao na ukosefu wa vifungashio ataweka mikakati na wadau ili kuwa na kiwanda kidogo cha kutengeneza vifungashio vyenye ubora.

Upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya open mind and though organizasion (OMTO) Anna Haule alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwafanya wanawake kujitambua ili kujikwamua kiuchumi ili wafanye siasa wakiwa na uchumi.

 Nae Mkurugenzi wa shirika la Road-to-success  Rodrick Nabe aliwataka wanawake viongozi wa UWT ngazi ya Kata kutoa hamasa ya wanawake kujiunga katika vikundi na kuanzisha ujasiriamali.

Akieleza  mjasiriamali ambae pia ni mwenyekiti wa UWT Kata ya Bulega Rahabu Ngukulu kwenye mafunzo ya ujasiriamali yaliyokuwa yanatolewa kwa wenyeviti na makatibu wa UWT kata zote 17 za Wilaya ya Bukombe ambayo ni namna ya kutengeneza pafyumu,pilipili sosi, Sabuni ya mche kwa kutumia mchele.

 Ngukulu alisema wanawake wengi wamekuwa wakishindwa kuazisha ujasiriamali kutokana na maisha duni na kuwa tegemezi kwa wanaume kuendesha familia.

Pia Elizabeth Paul alisema mafunzo hayo ya ujasiriamali yamempa mwanga na kufikiri kuboresha biashara yake ya kutengeneza sabuni ya kufulia kwa kutumia mchele.
Wakati huo huo Mbunge Chagulla alikabidhi msaada wa shuka 100 kwa ajili ya wodi ya wazazi ya mama na mtoto katika hospitali ya Wilaya ya Bukombe.

Comments