Baada
ya golikipa Juma Kaseja kufanikiwa kuipatia Taif Stars ushindi wa
penati 3-0 na kuingia hatua ya makundi ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia
2022 nchini Qatar, Juma Kaseja ndio alikuwa shujaa wa mchezo huo baada
ya kucheza penati ya kwanza iliyoleta nguvu kwa Taifa Stars na
kuwadhoofisha Burundi, kiasi cha RC Makonda kumtangazia zawadi nono.
RC
Paul Makonda leo hii ametimiza ahadi yake ya kumpa zawadi ya Tsh
Milioni 10 golikipa Juma Kaseja baada ya kumtangaza kama nyota wake wa
mchezo wa jana kati ya Tanzania dhidi ya Burundi, game hiyo iliisha kwa
Tanzania kushinda kwa penati 3-0.
Tanzania ilicheza game hiyo na
dakika 120 kumalizika kwa sare ya kufungana magoli 1-1, goli la Tanzania
likifungwa na Mbwana Samatta dakika ya 30 huku la Burundi likifungwa na
Feiston dakika za nyongeza kabla ya kwenda mapumziko, mikwaju ya penati
ndio iliamua timu ipi isonge mbelee baada ya kuwa na aggregate ya 2-2.
Comments
Post a Comment