MWENYEKITI WA UVCCM-BUKOMBE AMUANIKA MHE. BITEKO

 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, Nelvin Salabaga amempongeza Mbunge wa Jimbo hilo ambae pia ni Waziri wa Madini Mhe. Doto Mashaka Biteko kwa kutoa Mifuko 50 ya saruji yenye thamani ya Tsh milioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa choo cha wanafunzi shule ya msingi Nampangwe. 


Salabaga aliyasema hayo wakati akizungmuza na wajumbe wa halmashauri kuu ya ccm kata ya Runzewe Mashariki baada ya kupata taarifa za Mbunge huyo kutoka kwa Katibu wa Ccm Kata hiyo kuwa Mbunge anashiriki kikamilifu kwenye miradi ya maendeleo inayo anzishwa na wananchi na miradi mingine kuwezesha bila nguvu za wananchi.

“Mhe. Biteko alitoa Tsh milioni 6 kujenga Zahanati ya Ikuzi, Tsh milioni 3 kwa ajili ya ukamilishaji wa madarasa shule ya Sekondari Msonga huku mifuko 100 ya saruji shule ya msingi Bulumbaga” Alisema Salabaga. 
 
Salabaga aliongeza kuwa Mbunge huyo ni kiongizi anae tambua uwajibikaji wa nafasi yake ya uwakilishi kwa wananchi na kutekeleza ilani ya ccm na kwamba amekuwa akijitoa michango mingi ya kuwaunga mkono wananchi wanaokuwa tayari kujiletea maendeleo.

Kwa nyakati tofauti Salabaga akiwa kata ya Butinzya akiwa anazungumza kwenye Halmashauri Kuu ya Ccm Kata alikuta Mhe. Biteko amechagia Tsh milioni 5 shule ya msingi Mbula na mifuko 100 ya saruji kwa ajiri ya ukarabati wa madarasa 4 na ofisi ya utawala shule ya msingi Ngita huku katika shule ya msingi Mbula Mbuge alitoa Tsh milioni 4 .5 kwa ajili ya kupaua na kukamilisha majengo ya shule hiyo.

Salabaga aliendelea kumwaga sifa za Mbunge huyo kuwa katika ukamilishaji wa madarasa shule ya msingi Isemabuna Mhe. Biteko alichangia Tsh milioni 2.5 huku Zahanati ya Butinza alitoa mifuko 100 ya saruji ili kuunga mkono nguvu za wananchi na Kijiji cha Silamila kwenye ujenzi Zahanati amechangia Tsh milioni 3.

Mbunge Biteko akizungumuza na blog ya Bukombesasa  kwa njia ya simu akiwa Dodoma Bungeni Mhe. Biteko alisema lengo lake la kuunga mkono nguvu za wananchi ni kuwa na dira ya kuibadilisha Bukombe.

Biteko aliongeza kuwa atahakikisha anaendelea kuwaunga mkono viongozi wa serikali kuanzia ngazi ya chini wa nao hamasisha miradi ya maendeleo ili kuleta mabadiliko ya kimaendeleo Wilayani Bukombe.
 
Diwani wa Kata ya Butinzya Mhe. Amos Shimo akizungumuza yake toka moyoni alimpongeza Mbunge Biteko kwa kumpa kilomita nyingi za kufungua barabara mpya za kuunganisha Kijiji cha Butinzya,Mubula hadi  Igwamanoni na Butinzya,Ngita, hadi Kata ya Ng’anzo.

Shimo alisema nguvu za Mbunge  Biteko ameziona pia kwenye kukamilisha kwa kupaua maboma yote ya madara ya shule ya msingi na sekondari yaliyokuwa yamekwa kwa muda mrefu hapo Katani.
  


Comments