Mgeni rasmi katika ufunguzi huo Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania CWT Mkoa wa Geita John Kafimbi
Ligi ya mwalimu Doto
cup 2019 yaanza kutimua vumbi Wilayani Bukombe Mkoa wa Geita huku timu ya Walimu Ushirombo fc imewachapa bao 4-1
Timu ya Walimu Igulwa fc katika mashindano ya ufunguzi wa Ligi ya Mwalimu Doto Cup
2019 katika uwanja wa Ushirombo
Sekondari.
Wafugaji wa Timu ya Walimu Ushirombo fc ni Mwalimu Medisoni
Mwaipopo dakika ya 34 na 44 goli la tatu Mwalimu Mjuni Mulugo alitupia dakika
ya 57 huku Bahati Kasante dakika ya 68.
Mfugaji wa Timu ya Walimu Igulwa fc Mwalimu George
Mbawala aliwapatiwa bao la kufutia
machozi Walimu wezeka dakika ya 85.
Huku katika mchuano wa Mwalimu Doto Cup katika Uwanja wa Bufanka kati ya Walimu Bugelenga fc 4-3 dhidi ya timu ya Walimu Iyogelo fc kwa
mikwaju ya penaliti baada ya kutoka sale dakika 90 ikiwa timu ya Walimu
Bugelenga imefuzu kusonga mbele.
Mgeni rasmi katika ufunguzi huo Katibu wa Chama cha Walimu
Tanzania CWT Mkoa wa Geita John Kafimbi amesema lengo la michezo hiyo ni
kuwaunganishwa walimu na kusisitiza kuwa kitendo alicho kifanya Mbunge wa Jimbo
la Bukombe Doto Mashaka Biteko kuazisha Ligi ya Mwalimu Doto Cup ni jambo jema alilolifanya
la kuwakumbuka walimu wezake.
Kafimbi ameongeza kuwa michezo ni Afya na fursa ya kupata
marafiki wapya pamoja na kuongeza
uimarishaji wa vipaji mashuleni.
Comments
Post a Comment