MHE BITEKO "VIONGOZI WA DINI HAMASISHENI WANANCHI KUWEKEZA KWENYE ELIMU"



Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita Mhe. Doto M. Biteko amewaomba viongozi wa madhehebu ya dini kuhamasisha wananchi kuwekeza kwenye Elimu ya watoto wao.

Biteko aliyasema hayo kwenye hafla ya harambee ya kuchangia michango ya hiyari kwa ajili ya ununuzi wa vyombo vya muziki Kanisa la Afirican Inlad Church A.I.C Ushirombo Wilaya ya Bukombe.
 
 “Ili kunufaika na Umoja wa Afrika Mashariki inayoundwa na Nchi 5 pamoja na  Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi 16 za Kusini mwa Afrika (SADC) ambao Mwenyekiti wake kwa sasa ni Rais Dk. John Magufuli inatakiwa wananchi wa Wilaya ya Bukombe kuwekeza kwenye Elimu na si vinginevyo ili kuwanusuru watoto wao kuwa watumwa wa wageni ” alisema Biteko.

 Biteko akikabidhi Tsh milioni 1 kwa ajili ya changizo la ununuzi wa vyombo vya mziki kanisani hapo, aliwaomba wananchi kila mtu kwa imani yake  aendelee kumuombea Rais Magufuli na wasaidizi wake ili Mungu Aendelee kuwapa hekima busara na maarifa zaidi waendelee kulitumikia Taifa letu.
 
Kwa upande wake Mchungaji wa Kanisa la Afirican Inland Church (A.I.C  Adamu Nzoka alisema wananchi kwa sasa wamekua na mwamko wa kusomesha watoto wao kutokana na serikali ya awamu ya tano kutoa Elimu Bure kuanzia darasa la awali hadi kidato cha Nne.
  
Nae muumini wa kanisa hilo Yohana Kasongi alisema Elimu ambayo imetolewa na Mbunge nihamasa ambayo itasaidia wananchi kufikisha ujumbe kwenye jami ili wawekeze kwenye Elimu.
 
 

Comments