DC APIGA MARUFUKU WANAFUNZI KUINGIA KUMBI ZA STAREHE

 
Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mkoa wa Geita, Said Nkumba amepiga marufuku wanafunzi kuingia kwenye kumbi za starehe ili kulinda maadili wanapo kuwa shuleni na kwenye jamii ikiwa shule ya sekondari Ushirombo ina  wanafunzi 1658 kati yao 14 wamesimamishwa masomo na uongozi wa shule hiyo kwa kosa la uvutaji wa madawa ya kulevya na kufanya uhalifu wakuteka wenzao huku wengine wakifanya biashara ya ngono.

Nkumba alitoa agizo hilo kwenye kikao cha wazazi na walezi wa shule ya sekondari Ushirombo baada ya Mwalimu wa nidhamu shule ya sekondari Ushirombo Happyness Charles kusema Ofisi yake kwa kufuata sheria na mioungozo ya shule wanafunzi 14 wamesimamishwa masomo kwa siku 21 tangu Agosti 11 na siku zinaisha wakati huu walikizo fupi hadi Sepetmba 16 shule ikifunguliwa bodi itakuwa imekaa na kuchukua maamzi stahiki kwa wanafunzi hawo.

Charles alisema kati ya wanafunzi waliosimamishwa 14 kati yao wavulana 12  msichana 1 kwa makosa mbali mbali likiwemo la kuvuta dawa za kulevya na msichana 1 amesimimishwa kwa kufanya biashara ya kujiuza mwili wake.
  
“Agizo la serikali ya Wilaya litasaidia wanafunzi kutopata vishawishi vya utumiaji madawa ya kulevya na mavazi yasiyo ya kimaadili kwa wasichana na wavulana hasa nguo za kubana (modo) na kwamba wanafunzi wengi wamekuwa wanaingia kwenye kumbi za starehe kwa ruhusa ya wazazi na walezi kwenda kudansi shoo kwenye kumbi za harusi” alisema Charles

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Bukombe Philibert Nyangahondi aliwaomba wazazi na walezi kushirikiana na walimu kuwajengea uwezo wa kiutamaduni wa maadili mema na kuhakikisha wanafuatilia maenedeleo ya wanafunzi mashuleni. 

Nkumba aliagiza bodi ya shule kukaa kikao na kuhakiki upya majina ya wanafuzi septemba 10 ikiwa ni kabla ya likizo fupi kuisha na watakao bainika wanahatia  wafukuzwe shule.
Nkumba akitoa angizo kwa Mkuu wa Polisi Wilaya Elisha Kusula kuhakikisha siku 30 anakamata wauzaji wa bangi, na wamiliki wa bar wanaotoa ajira kwa wanafunzi na kufanya dolia ya mara kwa mara.
Nae Kusula alisema atatekeleza maagizo siku 30 ni nyingi atakuwa amesafisha mji wa Ushirombo.
 “situmi mtu”alisema Mkuu wa Polisi Wilaya.

Miongoni mwa wazazi waliokuwa wamehudhuria kikao hicho Scholastika  Zefania  alisema chanzo cha wanafunzi kujiingiza kwenye tabia ya uvutaji bangi na kujiuza chanzo ni wazazi hasa wa kiume wamekuwa wakitelekeza familia na kuazisha nyumba ndogo na mzingo kubaki kwa akina mama.

Mohamed Hames alisema chanzo cha madili kuporomoka ni wanawake wamekuwa wakivaa nguo zisizo na maadili na kusifiana mbele ya watoto wao hali ambayo inawaadhirili watoto kujiingiza kwenye tabia mbovu shuleni na jamii kwa ujumla.

Comments