BUSELESELE FC YATWAA UBINGWA WA KAREMAN CUP 2019

Timu ya Buselesele fc yatwa ubingwa kwa kuibuka naushindi wa mabao 4-1 timu ya Kibehe fc mchuano wa fainali mashindano ya Karemani cup 2019 katika uwanja wa Chato wilayani chato mkoa wa Geita.
Mfungaji wa timu ya Buselesele fc goli lakwanza Emmanuel Shimla dakika ya 39 huku goli tatu yakifungwa kwa mikwaju ya penaliti baada ya dakika 90 kuisha timuzote zikiwa sale ya 1-1 mfugaji wa goli la Kibehe fc Ezekiel Kalisho dakika ya 78 huku timu hiyo katika mikwaju ya penaliti haikufunga hata goli moja nakuipa Buselesele fc ubingwa.
Katibu mkuu chama cha mpira wa miguu wilaya ya Chato (CDFA) Wilfred Machugu amesema kuwa mashindano hayo yalianza Juni 20 na fainali imefanyika Septemba 15 mashindano hayo yalishirikisha timu 115 namichuano ilianzia ngazi ya vijiji kata tarafa hadi wilaya.
Machugu alisema lengo la ligi hiyo nikuibuwa vipaji na kuhakikisha wanapata timu itakayo shiriki daraja la tatu hadi la kwanza na kunawachezaji 10 wamesha chukuliwa na timu ambazo zinashiriki ligi kuu Biashara Unaited, Kagera shuga.
 Mshindi wa kwanza timu ya Buselesele fc ambao nimabingwa walitwa kitita cha fedha sh 1 milioni na ng’ombe wawili jezi seti mbili na mpira mmoja huku mshindi wa pili Kibehe fc wakibeba sh 700,000 na mbuzi wa wili jezi seti moja mpila mmoja, mshindi wa tatu Nyuki fc alibeba sh 500,000 na jezi seti moja na mpira mmoja huku mshindi wa nne timu ya Selengeti fc aliambulia sh 300,000 jezi seti moja na kuku wa wiili.
Akikabidhi dhawadi hizo mkuu wa mkoa wa Geita Robart Gabriel aliwataka vijana kuendeleza vipaji vyao na sio kujiingiza kwenye makundi mabaya ambayo yanaweza kuhatalisha maishayao na kwamba michezo ni ajira na inajenga urafiki na afya pia.
Mzamini wa mashindano hayo mbuge jimbo la chato ambae pia waziri wa nishati Dk Edward Kareman alisema kaulimbiu ya mashindano hayo nikuhamasisha wananchi kujitokeza kupiga kura kuchaguwa kiongozi bora wakuwaletea maendeleo katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakao fanyika mwishoni mwa mwaka huu.
Fainali za mashindano hayo yalihudhuliwa na mbunge wa jimbo Bukombe ambae pia waziri wa madini Doto Biteko na mbunge wa jimbo l a Geita mjini ……Kanyasu na viongozi wengine mbali mbali huku uwanja ukiwa umefulika mamia ya wananchi.
kama kawaida yetu mashabiki


Mchuano ikiendelea uwanjani 

Mhe Medard Kalemani ambae ni mbunge wa jimbo la chato ambae pia ni mdhamini wa mashindano ya Kalemani cup 2019

Mkuu wa mkoa wa geita Mhe. Mhandisi Robert Luhumbi akikabidhi zawadi kwa washindi
Mkuu wa mkoa wa geita Mhe. Mhandisi Robert Luhumbi akizungumza jambo na wabunge waliohudhuria kwenye mashindano
Kama Kawaida yetu mashabiki

Mhe.Constantine Kanyasu ambae ni mbunge wa Geita Mjini akizungumza jambo baada ya kumalizika kwa mashindano

Mhe Doto Biteko katika juhudi za kuunga mkono katika fainali ya Kalemani cup
Mhe Doto Biteko katika juhudi za kuunga mkono katika fainali ya Kalemani cup
Mhe Doto Biteko katika juhudi za kuunga mkono katika fainali ya Kalemani cup


Comments